Skip to main content

Posts

Showing posts from January, 2021

UKOSEFU WA HAMU YA TENDO LA NDOA (LIBIDO LOSS)

 UKOSEFU WA HAMU YA TENDO LA NDOA low sex drive Ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa ni changamoto ambayo inawakumba watu wengi, wanaume kwa wanawake katika wakati flani wa maisha yao. Ingawa visababishi vyake vinaweza kutofautiana baina ya mtu na mtu, Afya njema ya maisha ya tendo la ndoa hutegemea sana ulaji mzuri, ufanyaji kazi mzuri wa mishipa ya fahamu, kiwango sahihi cha vichochezi (hormones) pamoja na damu kuzunguka vizuri kwenye mishipa iliyopo maeneo ya pelvis (kwenye nyonga).  VISABABISHI VYA UKOSEFU WA HAMU YA TENDO LA NDOA KWA WANAWAKE Matatizo ya Uzazi: kama vile maumivu wakaji wa tendo,  Baadhi ya magonjwa: kama vile saratani, kisukari, shinikizo la juu la damu (hypertension),  Baadhi ya dawa: kama vile anti depressants husababisha ukosefu huu. Upasuaji: wa sehemu ya matiti au maeneno ya sehemu za siri. Uchovu: majukumu mengi ya kina mama huwafanya wachoke sana na hivyo kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa. Kukoma kwa hedhi (menopause): kipindi hiki estrogen hupungua sana

SHINIKIZO LA JUU LA DAMU/HIGH BLOOD PRESSURE

 SHINIKIZO LA JUU LA DAMU/HIGH BLOOD PRESSURE Shinikizo la juu la damu(hypertension) NINI MAANA YA SHINIKIZO LA JUU LA DAMU? Hii ni hali ambayo msukumo wa damu kwenye kuta za mishipa ya damu ni mkubwa sana kuliko kawaida. kwa kawaida, inasemekana mtu ana shinikizo la juu la damu kama pressure yake kwenye vipimo ni kuanzia 140/90 mmhg au zaidi. Na hua inasemekana kua pressure imezidi sana kama pressure yake kwenye vipimo ni zaidi kuanzia 180/120 mmhg au zaidi. Kwa kawaida mtu anaweza asionyenye dalili za kua na pressure mwanzoni, ila ikiendelea kwa muda flani bila kufanya juhudi za kuishusha, basi atapata magonjwa ya moyo na ndipo ataanza kuonyesha dalili za kua na pressure. Na kama dalili zikitokea, basi hua ni kusumbuliwa na maumivu ya kichwa mara kwa mara, kukosa pumzi, kutokwa na damu puani.  NINI HUSABABISHA SHINIKIZO LA JUU LA DAMU? kuna baadhi ya magonjwa au sababu za kiafya zinazoweza kusababisha shinikizo la juu la damu, kama vile magonjwa ya figo, utumiaji wa dawa hatarishi, m

VIDONDA VYA TUMBO (ULCERS)

 NINI CHA KUFANYA KAMA UNA VIDONDA VYA TUMBO (ULCERS) Peptic Ulcer VIDONDA VYA TUMBO NI NINI? Vidonda vya tumbo ni tatizo linalotokea pale ambapo kuta za tumbo kua na vidonda. Hii hutokea baada ya kuharibika kwa ute (mucus) ambao hulinda kuta za tumbo. Ute huu huharibiwa na acid ambayo hua inamwagika tumboni kwa lengo la kuyeyusha chakula na kuua vijidudu visivyotakiwa kwenye chakula.  AINA ZA VIDONDA VYA TUMBO. 1 .Vidonda vya kwenye Tumbo (Gastric ulcers) : Hivi hutokea ndani ya tumbo. Gastric/stomach ulcers 2. Vidonda vya kwenye Utumbo (Duodenal Ulcers): Hivi hutokea kwenye utumbo. Duodenal Ulcer NINI HUSABABISHA VIDONDA VYA TUMBO? Bakteria waitwao Helicobacter Pylori (H.pylori) Matumizi ya mara kwa mara ya dawa za maumivu kama vile Aspirin na NSAIDs nyingine. Uvutaji wa sigara Kua na msongo wa mawazo Unywaji mkubwa wa pombe Saratani ya tumbo Visababishi vingine kama vile kukaa muda mrefu bila kula chakula. NI DALILI ZIPI ZA VIDONDA VYA TUMBO? Maumivu makali ya tumbo (kama kuunguza

UZITO ULIOZIDI/OBESITY/KITAMBI/NYAMA ZEMBE

  OBESITY/ UZITO ULIOZIDI, NINI MAANA YAKE? Obesity ama unene, uzito uliopitiliza ni ugonjwa unaohusisha mwili kua na mafuta mengi kuliko kiwango kinachotakiwa. Hali hii sio kwamba inakupa mwonekano mbaya tu, bali ni hali inayoongeza hatari ya magonjwa kama vile magonjwa ya moyo, kisukari, shinikizo la juu la damu pamoja na aina kadhaa za saratani. UTAJUAJE KAMA UZITO WAKO UMEZIDI? (OBESITY) Wataalam walikuja na kitu kinachoitwa BODY MASS INDEX, (BMI) . na wakaonyesha ya jinsi unavyoweza kujua kama una uzito sahihi kulingana na Urefu pamoja na uzito ulio nao. FORMULAR YA BMI BMI hutafutwa kwa kutumia uzito wako kwa kg pamoja na urefu wako kwa mita. hivyo kama una urefu mfano wa cm 170, basi utabadilisha ziende kua meter. ambapo cm 170 ni sawa na 1.7m Hivyo BMI ni sawa na uzito wako kwa kg gawanya kwa mraba wa urefu kwa meter. BMI = kg/m2 lakini ni rahisi zaidi kujua BMI yako kwa kutumia mtandao. utaenda sehemu ya Google na uandike BMI CALCULATOR . itakupeleka sehemu husika ya kupata

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (°C). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI?  Kwa kawaida, mwanaume anahitaji Calorie 250

APPLE CIDER VINEGER KWENYE KUPUNGUZA UZITO.

  Apple Cider Vineger UKWELI KUHUSU APPLE CIDER VINEGER KUPUNGUZA UZITO. Kwa miaka mingi, Apple cider vineger (siki ya tufaa) ilikua ikitumika kama dawa ya vitu vingi kama vile kupunguza kiwango cha sukari mwilini pamoja na kupunguza kiwango cha lehemu n.k Japokua hamna tafiti za moja kwa moja zinazohusisha siki ya tufaa kupunguza uzito, watu watu kadhaa ambao wanasema imewasaidia kwa kiasi flani ukilinganisha na ambao hawakua wakitumia siki ya tufaa. BAADHI YA FAIDA ZITOKANAZO NA KUTUMIA SIKI YA TUFAA . Husaidia kuweka sawa mmeng,enyo wa chakula Husaidia kushusha kiwango cha sukari kwa wenye kisukari Husaidia kupunguza lehemu mbaya (bad cholesterol) Husaidia kuondoa kiungulia Inasaidia kufanya detox Na faida nyingine nyingi JINSI YA KUTUMIA SIKI YA TUFAA (APPLE CIDER VINEGER) KUPUNGUZA UZITO. Andaa glass au kikombe kimoja cha maji ya kunywa. weka vijiko viwili vya chakula vya maji ya limao/ndimu weka vijiko viwili vya chakula vya Apple Cider Vineger weka kijiko kimoja cha chakula cha

NINI MKAKATI WAKO WA KUA NA UZITO SAHIHI/AFYA BORA MWAKA 2021?

  UNA MKAKATI GANI ILI KUA NA UZITO SAHIHI 2021? kuna msemo hua napenda sana kuutumia, ya kwamba MJI WA ROMA HAUKUJENGWA KWA SIKU MOJA. Hii inamaanisha ya kwamba, afya ya mtu ilivyo, ni matokeo ya alivyozoea kula kwa kipindi cha muda flani. Hamna mtu aliyenenepa kwa siku moja, wala aliyepungua kwa siku moja. ila vyote huhusisha mazoea ya namna flani ambayo ndio husababisha mtu kua na afya ya namna flani. Mara nyingi watu hupenda sana kupungua ndani ya muda mfupi, tena bila kuweka juhudi katika kupungua, lakini wanasahau ya kwamba, hata unene walionao haukuja kwa muda mfupi. Bali umechukua muda flani wao kufikia unene huo waliokua nao. Ili uweze kua na uzito sahihi (uzito sahihi hukufanya kuepukana na magonjwa mengi yasioambukizwa ambayo ni hatarishi), Ni lazima uanze kufanya baadhi ya vitu. lakini sio kufanya tu, inabidi viwe tabia yako ya kila siku. Na endapo vitu hivyo vikiwa tabia, basi ndani ya muda flani Afya yako itaimarika zaidi na zaidi. TABIA 10 AMBAZO ZITAKUWEZESHA KUA NA UZI