Skip to main content

UKOSEFU WA HAMU YA TENDO LA NDOA (LIBIDO LOSS)

 UKOSEFU WA HAMU YA TENDO LA NDOA

low sex drive

Ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa ni changamoto ambayo inawakumba watu wengi, wanaume kwa wanawake katika wakati flani wa maisha yao.

Ingawa visababishi vyake vinaweza kutofautiana baina ya mtu na mtu, Afya njema ya maisha ya tendo la ndoa hutegemea sana ulaji mzuri, ufanyaji kazi mzuri wa mishipa ya fahamu, kiwango sahihi cha vichochezi (hormones) pamoja na damu kuzunguka vizuri kwenye mishipa iliyopo maeneo ya pelvis (kwenye nyonga). 

VISABABISHI VYA UKOSEFU WA HAMU YA TENDO LA NDOA KWA WANAWAKE


  • Matatizo ya Uzazi: kama vile maumivu wakaji wa tendo, 
  • Baadhi ya magonjwa: kama vile saratani, kisukari, shinikizo la juu la damu (hypertension), 
  • Baadhi ya dawa: kama vile anti depressants husababisha ukosefu huu.
  • Upasuaji: wa sehemu ya matiti au maeneno ya sehemu za siri.
  • Uchovu: majukumu mengi ya kina mama huwafanya wachoke sana na hivyo kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa.
  • Kukoma kwa hedhi (menopause): kipindi hiki estrogen hupungua sana na baadhi hupoteza hamu kabisa na kua na uke mkavu.
  • Ujauzito au wakati wa kunyonyesha: hua na mabadiliko ya hormones zinazoweza kupelekea kupungua kwa hamu.
  • Matatizo ya kisaikolojia: kama vile historia ya unyanyasaji wa kijinsia, kujiona kua na shepu mbaya, pamoja na msongo wa mawazo, au ugomvi usioisha kwenye mahusiano.

VISABABISHI VYA UKOSEFU WA HAMU YA TENDO LA NDOA KWA WANAUME.

  • Kupungua kwa Testosterone: Hii ndio hormone inayojulikana kwa UWANAUME
  • Baadhi ya Dawa: mfano dawa za presha huchangia kupungua kwa Hamu ya tendo.
  • Msongo wa mawazo: hupelekea kushuka kwa testosterone.
  • Magonjwa: kama vile Kisukari, Shinikizo la juu la damu (pressure), matatizo ya figo na ini.
  • Uzito uliopitiliza: ni moja ya visababishi vya upungufu wa nguvu za kiume.
  • Kutokupata usingizi wa kutosha: hupelekea kushuka kwa testosterone.
  • Uzee: kadri umri unavyozidi kwenda, kiwango cha testosteron hupungua.
  • Unywaji wa pombe kupita kiasi.
  • Uvutaji wa Sigara na dawa za kulevya.
  • Kukosa kujiamini (kisaikolojia).

NINI CHA KUFANYA?




  • Punguza matumizi ya wanga uliokobolewa: penda sana kutumia wanga ambao haujakobolewa, chakula jamii ya kunde, matunda pamoja na mboga mboga. Tumia pia kiwango cha kutosha cha protini. Matunda jamii ya machungwa ni mazuri kwa ajili ya Vitamin C ili kuimarisha kuta za mishipa ya damu. Mboga za majani zina Riboflavin kwa ajili ya kuleta ute kwenye uke wa mwanamke.
  • Tumia Zinc: Husaidia sana katika mambo ya afya ya uzazi, inahusika hata katika utengenezwaji wa shahawa. Inapatikana zaidi kwa viumbe vya baharini (seafood), nyama, kuku, maini, mayai, maziwa, maharage, pamoja na nafaka ambazo hazijakobolewa.
  • Punguza matumizi ya pombe: ukitumia kupita kiasi, husababisha kusinyaa kwa korodani na upotevu wa nguvu za kiume.
  • Tumia madini ya chuma: hupatikana kwenye nyama, samaki, mbegu (karanga), jamii ya kunde, nafaka ambazo hazijakobolewa, matunda na mboga za majani.
  • Tumia kitunguu swaumu kama kiungo: unga chakula chako bila kukosekana kwa kitunguu swaumu mara kwa mara. kina allicin inayosaidia katika mzunguko wa damu katika viungo vya uzazi kwa wanawake na wanaume.
  • Fanya mazoezi: ili uzalishe hormone ya endorphin, kua na uzito sahihi pamoja na kusaidia mzunguko wa damu.
  • Usivute Sigara: Nicotine ni adui wa mishipa ya damu. husababisha kutengenezeka kwa plaque kwenye mishipa ya kwenye uume pamoja na kusinyaa.

kwa msaada zaidi juu ya Tiba ya ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa/ urijali au upungufu wa nguvu za kiume. Tuwasiliane. Bonyeza HAPA kwa whatsapp.

MAWASILIANO:

0753068572 (Mobile)
0621068072 (whatsapp)

Imeandikwa na SAMUEL MACHA
FIT BY WAYNE.

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed