Skip to main content

UZITO ULIOZIDI/OBESITY/KITAMBI/NYAMA ZEMBE


 OBESITY/ UZITO ULIOZIDI, NINI MAANA YAKE?

Obesity ama unene, uzito uliopitiliza ni ugonjwa unaohusisha mwili kua na mafuta mengi kuliko kiwango kinachotakiwa.

Hali hii sio kwamba inakupa mwonekano mbaya tu, bali ni hali inayoongeza hatari ya magonjwa kama vile magonjwa ya moyo, kisukari, shinikizo la juu la damu pamoja na aina kadhaa za saratani.

UTAJUAJE KAMA UZITO WAKO UMEZIDI? (OBESITY)

Wataalam walikuja na kitu kinachoitwa BODY MASS INDEX, (BMI). na wakaonyesha ya jinsi unavyoweza kujua kama una uzito sahihi kulingana na Urefu pamoja na uzito ulio nao.

FORMULAR YA BMI

BMI hutafutwa kwa kutumia uzito wako kwa kg pamoja na urefu wako kwa mita. hivyo kama una urefu mfano wa cm 170, basi utabadilisha ziende kua meter. ambapo cm 170 ni sawa na 1.7m

Hivyo BMI ni sawa na uzito wako kwa kg gawanya kwa mraba wa urefu kwa meter.

BMI = kg/m2

lakini ni rahisi zaidi kujua BMI yako kwa kutumia mtandao. utaenda sehemu ya Google na uandike BMI CALCULATOR. itakupeleka sehemu husika ya kupata BMI yako. Au bonyeza BMI CALCULATOR

au unaweza kupakua application kutoka playstore au appstore inayoitwa BMI calculator na kisha ukaitumia kupata BMI yako kwa urahisi.

chati ya BMI

BMIHali ya Uzito
Pungufu ya 18.5uzito wa chini (Underweight)
18.5-24.9Uzito wa kawaida (Normal)
25.0-29.9Uzito uliopitiliza (Overweight)
Zaidi ya 30.0 Unene (Obesity)
NINI HUSABABISHA UZITO MKUBWA, KITAMBI AU NYAMA ZEMBE?

Japokua kuna sababu za Genetics, Hormones, Tabia, pamoja na Mazingira. Kwa ujumla Obesity Husababishwa na mtu Kuingiza Calorie nyingi mwilini kuliko zile ambazo anazitumia kwa siku.

Ukitaka kufahamu zaidi kuhusu Calorie Bonyeza hapa CALORIE

VISABABISHI VYA UZITO MKUBWA/OBESITY.
  • Ulaji mbovu wa chakula: unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyochoma, hii husababisha kuongezeka kwa uzito, kitambi pamoja na nyama zembe. 
  • kutokushughulisha mwili: hii husababisha mwili kukusanya calorie nyingi bila kuzichoma, na matokeo yake kuhifadhiwa kama mafuta.
  • Ujauzito: kwa baadhi ya wanawake ujauzito huwasababishia kuongezeka uzito.
  • Kutokupata usingizi wa kutosha: hii hupelekea mabadiliko ya hormones kwenye mwili wako na kupelekea kunenepa.
  • Msongo wa mawazo: pia husababisha mabadiliko ya hormones, hivyo kuongezeka uzito.

MADHARA YATOKANAYO NA KUA NA UZITO MKUBWA.
  • Kutokuishi muda mrefu kwa ujumla (mortality): tafiti zinaonyesha ya kwamba, watu wenye uzito mkubwa huishi muda mfupi zaidi ukilinganisha na watu wenye uzito sahihi.
  • Shinikizo la juu la damu (High blood pressure)
  • Kiwango kikubwa cha lehemu mbaya (LDL Cholesterol)
  • Kisukari
  • Ugonjwa wa moyo
  • Kiharusi (stroke)
  • Mawe kwenye kibofu cha mkojo
  • Matatizo ya mifupa na viungio (joints and bone problems)
  • Kukoroma wakati wa kulala na kushindwa kuhema vizuri wakati wa kulala.
  • Saratani za aina mbali mbali
  • Maumivu ya mwili na kupata shida kufanya movements za kawaida.
  • Na matatizo mengine mengi ambayo utaona yakiondoka pale ambapo mwili wako utakua na uzito wa kawaida.

JINSI YA KUJIKINGA/KUONDOKANA NA UZITO MKUBWA.

Awali ya yote, nipende kusema jambo moja. MJI WA ROMA HAUKUJENGWA KWA SIKU MOJA. wazungu hupenda kusema ROME WAS NOT BUILT IN ONE DAY.

Hii ina maana ya kwamba, hamna njia ya fasta fasta (MAGIC TRICK) ya kuondokana na uzito mkubwa, kwa sababu pia hakuna mtu aliyenenepa kwa fasta fasta. Bali ni matokeo ya mtindo flani wa kula pamoja na kuishi kwa muda flani.

Yawezekana ukatumia njia flani ya fasta fasta na ukaona unapungua. Lakini ukweli ni kwamba mwili wako unajiweka katika Energy saving mode. Mwili unakua unafanya hivyo ukihisi ya kwamba landa ni tatizo limetokea kwenye mwili wako. Hivyo utafanya hivyo ili uweze kukulinda. Baada ya muda flani, mwili wako unarudi kwa nguvu na kunenepa hata zaidi ya hapo awali.

Hivyo ni vyema kama unatamani kupungua, basi uwe tayari kubadilisha tabia na mtindo wako wa maisha. Unaweza kua unapungua kidogo kidogo, lakini ukakaa vizuri baada ya muda flani bila kuhofia kunenepa ghafla.

JINSI YA KUJIKINGA/KUONDOKANA 
  1. Punguza kiwango cha calorie: ukiweza kuongezea na mazoezi walau nusu saa kwa siku, hii itakusaidia kupunguza kilo 0.5 hadi 0.9 katika kila wiki.
  2. Usiache kupata Breakfast: tafiti zinaonyesha ya kwamba, watu waliokua wakipata breakfast walikua na uzito wa kilo 2.7 pungufu kuliko waliokua wanaruka breakfast kwa wanaume, na pungufu ya kilo 4 kwa wanawake.
  3. Tumia vyakula vyenye nyuzi nyuzi zaidi: hii ni kuacha kutumia vyakula vya wanga uliokobolewa na kutumia vyakula vya wanga ambao haujakobolewa.
  4. Tumia mboga mboga zaidi: unapopakua chakula chako, jaza zaidi mboga mboga na matunda kuliko wanga.
  5. Tumia vyakula vya protini katika kila mlo: sio lazima iwe protini ya wanyama ili kupunguza gharama, unaweza hata kutumia protini zitokanazo na mimea. kama vile maharage, mbaazi, kunde, njegere n.k
  6. Shughulisha mwili zaidi: hapa ni kuhakikisha unaweza kutembea zaidi badala ya kutumia usafiri au kitu kinachokusaidia kusogea, unaweza ukawa unatumia ngazi badala ya lift, ukienda kazini gari lako paki mbali kidogo ili uweze kutembea, tembea tu kwa dk 15 asubuhi na 15 jioni. au ukatembea kwa dk 30 kwa wakati mmoja, penda kufanya vitu mwenyewe badala ya kutuma wasaidizi n.k
  7. Fanya mazoezi walau mara 3 kwa wiki.
Hii ndio misingi mikubwa ya kuweza kupungua uzito au kua na uzito sahihi, ni vitu ambavyo vinatakiwa viwe kama tabia.
YOU ARE WHAT YOU EAT, yaani wewe ni matokeo ya kile unachokula.

Ikiwa utapenda kupata ratiba nzuri ya kula ili uweze kupungua uzito, wasiliana nami kwa whatsapp kwa kubonyeza KUPUNGUA UZITO

Imeandikwa na SAMUEL MACHA
FIT BY WAYNE.

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed