Skip to main content

VIDONDA VYA TUMBO (ULCERS)

 NINI CHA KUFANYA KAMA UNA VIDONDA VYA TUMBO (ULCERS)

Peptic Ulcer
VIDONDA VYA TUMBO NI NINI?

Vidonda vya tumbo ni tatizo linalotokea pale ambapo kuta za tumbo kua na vidonda. Hii hutokea baada ya kuharibika kwa ute (mucus) ambao hulinda kuta za tumbo. Ute huu huharibiwa na acid ambayo hua inamwagika tumboni kwa lengo la kuyeyusha chakula na kuua vijidudu visivyotakiwa kwenye chakula. 

AINA ZA VIDONDA VYA TUMBO.

1.Vidonda vya kwenye Tumbo (Gastric ulcers): Hivi hutokea ndani ya tumbo.
  1. Gastric/stomach ulcers

2.Vidonda vya kwenye Utumbo (Duodenal Ulcers): Hivi hutokea kwenye utumbo.
Duodenal Ulcer


NINI HUSABABISHA VIDONDA VYA TUMBO?
  1. Bakteria waitwao Helicobacter Pylori (H.pylori)
  2. Matumizi ya mara kwa mara ya dawa za maumivu kama vile Aspirin na NSAIDs nyingine.
  3. Uvutaji wa sigara
  4. Kua na msongo wa mawazo
  5. Unywaji mkubwa wa pombe
  6. Saratani ya tumbo
  7. Visababishi vingine kama vile kukaa muda mrefu bila kula chakula.
NI DALILI ZIPI ZA VIDONDA VYA TUMBO?
  1. Maumivu makali ya tumbo (kama kuunguza) mara baada ya kula au mda mwingine kabla.
  2. kiungulia
  3. kichefuchefu au kutapika (hali ikiwa mbaya zaidi unatapika damu)
  4. Tumbo kujaa gesi
  5. Kupata choo cheusi au chenye damu na harufu mbaya (hali ikiwa mbaya)
  6. Kutokupata hamu ya kula na kupungua uzito
NINI CHA KUFANYA KAMA UNA VIDONDA VYA TUMBO.
  1. Acha kutumia vyakula ambayo havifai kwa vidonda vya tumbo: Kwa kawaida, kuna tofauti baina ya mtu na mtu katika vyakula vinavyosumbua vidonda. ila ni vyema kuepuka vyakula vyenye caffein kama vile kahawa. epuka kula chocolate, pombe, pilipili pamoja na vyakula vinavyotengenezwa kutumia nyanya.
  2. Usile chakula usiku mwngi sana: kwa sababu ukila utafanya tumbo liachilie acid kwa ajili ya digestion wakati umelala.
  3. Punguza vyakula vyenye mafuta na maziwa: vyakula hivi husababisha tumbo kuchelewa kuondoa chakula na matokeo yake acidi kumwagika kwa wingi. Maziwa huondoa maumivu kwa muda, ila baada ya muda husababisha acid imwagike nyingi zaidi tumboni.
  4. Punguza matumizi ya viungo vikali: hivi husababisha acid kumwagika kwa wingi (increased gastric secretions). mfano pilipili, kitunguu swaumu, karafuu n.k
  5. Kula vyakula vyenye madini ya chuma: kwa sababu kama una vidonda ambavyo vinakusababishia kutoka damu kwa ndani, utapata kitu tunaita Irone deficiency Anemia. Hivyo tumia sana nyama ambayo haina mafuta, kuku au bata, mkate wa brown (epuka sana mkate mweupe. tumia wa brown ambao ngano yake haijakobolewa)
  6. Tumia maziwa ya mtindi: mara nyingi yana bacteria wanaofahamika kama live lactobacilli pamoja na bifidobacteria, hua wanapunguza kuumwa kwa vidonda hivi tumboni.
  7. Kunywa juice ya alovera ukiweza: nusu kikombe mara tatu kwa siku husaidia.
UKIACHILIA MBALI KWENYE MLO, EPUKA VITU HIVI...
  1. Usivute sigara: husababisha vidonda visipone na pia hufanya viwe vinajirudia kila wakati.
  2. Usitumie dawa za maumivu bila kupata ushauri wa mtu wa afya.
  3. Fanya mazoezi mara kwa mara ili kufanya Endorphin ipande: endorphine husaidia kuondoa maumivu mwilini. Hii ni kemikali ya kwenye ubongo
VYAKULA HATARISHI KWA VIDONDA VYA TUMBO
  • kahawa (au vinywaji vyote vyenye caffein)
  • pombe
  • pilipili
  • pilipili manga
  • nyanya
  • kitunguu swaumu
  • karafuu
VYAKULA VYA KUTUMIA VINAVYOSAIDIA.
  • Nyama isiyo na mafuta (lean meat)
  • mkate wa brown (ambao ngano yake haijakobolewa)
  • Vyakula jamii ya kunde (legumes)
  • Mtindi
VYAKULA VYA KUTUMIA KWA KIASI.
  • Vyakula vyenye mafuta
  • Maziwa
TIBA YA VIDONDA VYA TUMBO.
ikiwa unahitaji dawa ya vidonda vya tumbo, tafadhali bonyeza Hapa. WHATSAPP kisha utume neno VIDONDA VYA TUMBO

Imeandikwa na SAMUEL MACHA
FIT BY WAYNE.











Comments

  1. Mimi nasikia maumivu ya tumbo upande wa kushoto yanakuja mpaka mgongoni , nilipina nikaambiwa Sina shida, ila maumivu yanakuja na kupotea, yaani nahisi Moto unawaka kabisa.

    ReplyDelete
    Replies
    1. ebu tuwasiliane zaidi tujue tatizo ni nini. whatsapp 0621068572

      Delete

Post a Comment

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...