Skip to main content

Vidonda Vya Tumbo: Jinsi ya Kukabiliana na Kuvitibu.

 

Jinsi Ya Kukabiliana Na Kutibu Vidonda Vya Tumbo

Vidonda vya tumbo hutokea pale ambapo sehemu ya kuta za kwenye umio (Oesophagus),  tumbo au Utumbo kua na kidonda. Na hii hutokea baada ya kuharibika kwa Ute (mucus) ambao hulinda kuta hizo.

Unaweza kusoma zaidi kuhusiana na Vidonda Vya Tumbo na dalili zake kwa kubofya HAPA

Watu wengi hudhania ya kwamba bacteria anaefahamika kwa jina la H-pylori ni adui. Bacteria huyu sio adui yako, kwa sababu unaishi nae tangu siku unayozaliwa. Ila tu huleta shida pale ambapo tunakula lishe mbivu pamoja na mtindo mbaya wa maisha.

Ni Kwa Nini Vidonda Vya Tumbo Hutokea?

  • Matumizi ya pombe
  • Matumizi ya Nafaka (wanga) zilizokobolewa
  • Matumizi ya viungo vya kiwandani kama vile Royco
  • Matumizi ya Mafuta ya Mbegu (vegetable oils) mfano mafuta ya alizeti
  • Matumizi ya dawa za maumivu kama vile diclofenac na bufren
  • Matumizi mabaya ya dawa za antibiotics
  • Uvutaji wa sigara
  • Kutokupata usingizi wa kutosha
  • Kulakula hovyo au kila wakati (huvuruga uwiano wa uzalishwaji wa Hydrochloric acid tumboni)
  • Unene au Uzito uliozidi
  • Dawa za usingizi au za msongo wa mawazo (sonona), pamoja na dawa za presha

Nini Cha Kufanya Endapo Una Vidonda Vya Tumbo?

1. Kua Na Tabia ya Kufunga Kula

Mtindo wa 20:4 ni mwanzo mzuri katika tiba ya vidonda vya tumbo. 20:4 ni mtindo ambao unamaanisha ya kwamba utafunga kwa masaa 20 na utakula kwa masaa 4. (Kujua zaidi kuhusiana na jinsi ya Kufunga Bonyeza HAPA)

Unapofunga, utaruhusu kuta zilizochubuka kujitibu na kurudi katika hali yake ya kawaida. (regeneration)

Mkusanyiko wa Tindikali (acid concentration) hushuka na kua katika pH scale ya 1-3, na hivyo hufanya bacteria wa H-pylori asiwe adui, kuondoa bacteria hatarishi pamoja na kupona kwa oesophageal valve ambayo huzuia kucheua kwa gastric juice (juisi ya tumbo)

Kufunga kutasaidia pia uponyaji wa kibofu cha mkojo na hivyo kuzalishwa kwa Bile salts, na mwishowe kusaidia kuweka uwiano wa bacteria wazuri kwenye matumbo. (balance of gut bacteria)

2. Tumia Juice Ya Kabichi

Juisi ya Kabichi


Hii inatumika kama unashida yoyote ile kwenye tumbo au utumbo kama vile Vidonda vya tumbo, Ugonjwa wa Tumbo (gastritis), Diverticulitis, Gastroesophageal Reflux Disease (GERD) nakadhalika.

Kabichi ina glutamine ambayo husaidia kuponya Inflammation ya kwenye utumbo.

Mahitaji:

  • Kabichi ambayo ni fresh
  • Tango au Broccoli au vyote kwa pamoja
  • Karoti
  • Nazi
  • Chumvi

Jinsi ya Kuandaa:

  • Katakata kabichi yako, karoti pamoja na Tango au broccoli katika vipande vidogo vidogo
  • Weka kwenye blender na kisha usage kwa dakika moja
  • Chukua sehemu nyeupe ya nazi yako na uweke kwenye blender
  • Ongezea na Maji ya nazi yako pamoja na chumvi katika mchanganyiko wako.
  • Saga kwa dakika 2 au 3.

Matumizi:

Kunywa Juisi yako (mchanganyiko utakaoupata) muda ambao utakua unafungua au katika mlo wako wa kwanza wa siku. Na iwe masaa 3 au 4 kabla ya kwenda kulala.

(Kumbuka Utakua ukitumia mfumo wa kufunga wa 20:4, Hivyo Mlo wako wa mwisho unatakiwa uwe saa mbili usiku, na mlo wako wa kufungua utakua ni saa 10 jioni kesho yake. Na hapo utakua umefunga kwa masaa 20.)

Reference:


Imeandikwa na 
SAMUEL MACHA 
0753068572
0676068572
Endapo utahitaji tiba zaidi ya Vidonda vya Tumbo

FIT BY WAYNE

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed