Skip to main content

Mbinu za Kukusaidia Kua Mwanaume Rijali na Kuondokana na Upungufu wa Nguvu za Kiume

 

Mbinu Zinazosaidia Kua Mwanaume Rijali na Kuondoa Upungufu Wa Nguvu Za Kiume.

Upungufu wa nguvu za kiume (Erectile Dysfunction) ni hali ya kukosa uwezo wa kudumisha kusimama kwa uume wakati wa kufanya ngono.

Hali hii huleta fedheha ambayo huteteresha mahusiano yaliyo mengi, husababishwa na matukio au hali ambazo huvuruga utimamu wa misuli, vhichochezi (hormones), mishipa ya fahamu pamoja na mishipa ya damu katika uume.

Visababishi Vya Upungufu Wa Nguvu Za Kiume.

  1. Sababu za Kisaikolojia
  2. Sababu za kimetaboliki
  3. Sababu za mfumo wa neva za fahamu pamoja na mifupa ya misuli.

1. Sababu za Kisaikolojia

  • Sonona/ msongo wa mawazo
  • Unywaji wa pombe na sigara: (hudhoofisha mfumo wa neva, ubongo pamoja na mishipa ya damu kadiri mtumiaji anavyotumia)
  • Wasiwasi
  • Hali ya hatia
  • Kujiona huna thamani (low self esteem)
  • Picha ama video za ngono na punyeto: Hizi ndio mbaya zaidi kwani huleta ganzi katika sehemu zihusikazo na ladha za kimahaba katika ubongo.

2. Sababu Za Kimetaboliki

  • Ugonjwa wa kisukari
  • Shinikizo la juu la damu (High blood pressure/Hypertension)
  • Magonjwa ya tezi
  • Unene/uzito uliozidi.

3. Sababu Za Mifupa na Misuli

  • Unene/uzito uliozidi
  • Udhaifu wa misuli kama vile dystrophy
  • Magonjwa ya damu kama vile sickle cell
  • Magonjwa ya mishipa ya fahamu
  • Magonjwa mengineyo kama vile ngiri (hernia)

Dalili Za Upungufu Wa Nguvu Za Kiume

Kila mara unapojiandaa kwa ajili ya Tendo, unashindwa kudumisha kusimama kwa uume kwa lengo la tendo.

Kukosa kusimamisha uume mara tatu kwa siku pasipo kufanya au kufikiria jambo lolote lihusikanalo na ngono. kwa kawaida Mwanaume anatakiwa kusimamisha Uume wake mara tatu kwa siku, Asubuhi anapoamka, mida ya nyakati za mchana pamoja na Jioni. Na hii inatakiwa iwe inatokea akiwa hafikirii chochote kuhusiana na ngono.

Ni kutokana na mfumo wa kibaiolojia ujulikanao kama Circardian Rhythm

Ili Kupona Shida Ya Upungufu wa Nguvu Za Kiume

  • Kubali kwanza kama unatatizo, mshirikishe mwenza wako, usiogope, wewe ni mwanaume. wewe sio wa kwanza wala hutakua wa mwisho kua na tatizo hilo.
  • Hakikisha unatambua kisababishi kilichopelekea tatizo hilo na utatue
  • Acha kabisa matumizi ya pombe na sigara
  • Punguza unene kama unao.
  • Tibu magonjwa ya kimetaboliki kama unayo

Tiba Bora Zaidi Dhidi ya Upungufu Wa Nguvu Za Kiume.

  • Kula mlo safi (clean diet), ikiwa na maana ya kwamba usitumie kabisa sukari na vitu vya sukari.
  • Fanya mazoezi aina ya Strength Training au kunyanyua vitu vizito; itakupatia stamina, kupandisha kiwango chako cha homoni ya Testosterone pamoja na kuongeza uhai wa tendo la ngono.
  • Siku zote kua na mawazo chanya kama mwanaume.
  • Kunywa maji mengi ya kutosha kila siku
  • Usikose protini na mboga za majani katika mlo wako; protini huchochea uzalishwaji wa homoni ya testosterone pamoja na nyingine zihusikazo na afya ya uzazi.
  • Tembea juani haswa nyakati za asubuhi; utapata Vitamin D
  • Lala kwa walau masaa 7 kwa siku, itakuongezea urijali wako.
  • Oga maji ya baridi kila siku (usioge maji ya moto kama ni mwanaume)

Zingatia:

  • Usinunue dawa za kuongeza nguvu za kiume, hamna itakayokusaidia, badilisha mtindo wako wa maisha na utapona.
  • kupona huchukua muda, hivyo kua na subira. ROMA HAIKUJENGWA WA SIKU MOJA 
  • Unahitaji uthubutu, uthabiti na uvumilivu.
Kua mwanaume ambae Mungu alikuumba, kua na uume wenye nguvu na umridhishe mwanamke (mke) wako. Wanawake hupenda wanaume rijali.

Vyakula Ambavyo Kila Mwanaume Anapaswa Kuepuka.

  • Sukari (kama una watoto wa kiume waepushe na vitu vya sukari, ili waanze kua rijali mapema)
  • Unga wa ngano
  • Unga wa mahindi
  • Mafuta yatokanayo na mbegu (vegetable oils and seed oils)
  • Maziwa ya kiwandani
  • Energy drinks
  • Rangi ya chakula kama vile ubuyu, juice cola n.k
Vyakula tajwa hapo juu huharibu uwiano wa homoni ya testosterone vinapotumiwa mara kwa mara.

Uhusiano wa Homoni ya Testosterone, Urijali na Nguvu za Kiume.

Testosterone ni homoni ya kiume inayotengenezwa ndani ya korodani.

Ni kichocheo muhimu sana katika afya ya uzazi wa mwanaume pamoja na urijali wake. Ndio homoni inayohusika na Nguvu,  tamaa ya makuu (ambition), motisha, hamu ya tendo la ndoa pamoja na furaha. 

kwa kifupi ndio homoni inayompa mwanaume tabia za kiume endapo ipo katika kiwango sahihi.

Nini Hutokea Endapo Testosterone Ikiwa Pungufu?

  • Kukosa hamu ya tendo la ndoa
  • Upungufu wa nguvu za kiume
  • uchovu na kutokua na nguvu
  • Sonona

Vyakula Vinavyosababisha Kushuka kwa Testosterone

  • Sukari (kama una watoto wa kiume waepushe na vitu vya sukari, ili waanze kua rijali mapema)
  • Unga wa ngano
  • Unga wa mahindi
  • Mafuta yatokanayo na mbegu (vegetable oils and seed oils)
  • Maziwa ya kiwandani
  • Energy drinks
  • Rangi ya chakula kama vile ubuyu, juice cola n.k
  • Beer

Ni Kwa nini Mwanaume Anapaswa Kutokutumia Beer?

Beer ni Oestrogenic, ikiwa na maaana ya kwamba inafanyamageuzi ya kubadilika kwa testosterone kua Oestrogen (ambayo ni homoni ya kike). na kupelekea yafuatayo:-
  • Man Boobs (kua na matiti)
  • Unene
  • Hisia za kike (feminin emotions)
  • Kuongezeka kwa makalio na hips
  • Kupungua kwa hamu ya tendo
  • Upungufu wa nguvu za kiume na kuwahi kumwaga.
  • Ini lenye mafuta (Fatty liver)

Jinsi ya Kupandisha Kiwango cha Testosterone (kiwe na uwiano unaotakiwa)

  • Usitumie kabisa sukari au vitu vya sukari
  • Aacha kuangalia picha na video za ngono
  • Acha kupiga punyeto
  • Fanya tendo na mwanamke badala ya kuangalia porn na kujichua.
  • Fanya mazoezi ya kunyanyua uzito au aina ya HIIT
  • Tembea juani haswa nyakati za asubuhi
  • Lala kwa walau saa 8 au 7 kwa siku
  • Oga maji ya Baridi
  • kula nyama (isiwe imekaangwa/deep fried) na shahamu (fats) nzuri kama vile zeituni, nazi, parachichi, korosho, karanga, mlozi pamoja na mboga za majani haswa jamii ya kabichi kama vile kabichi, broccoli, cauliflower.
  • kua na tabia ya kumsifia mwanamke ambaye unadhani ni mzuri au anavutia. maneno kama Umependeza, wewe ni mzuri n.k: haimaanishi kwamba unataka kufanya nae ngono, hisia za ngono unaweza kufanya (transmute) kitu chanya.
  • Kua na tabia ya kufunga kula mara kwa mara. Wiki isiishe bila kufunga kula. unaweza kjifunza zaidi katika link hii JINSI YA KUFUNGA KULA
  • Tumia supu haswa ya kongoro au kichwa mara kwa mara: hua ina protini za kutosha na shahamu muhimu kwa ajili ya urijali.
  • Acha pombe kwani inaharibu uwiano wa testosterone.
  • Tumia boga mara kwa mara: lina wingi wa Vitamin A, Vitamin C, Vitamin K, madini ya Zince na Shaba ambazo ni muhimu sana kwa urijali.

Jinsi Ambavyo Kuoga Maji Baridi Husaidia Kuongeza Kiwango Cha Testosterone

Mwanaume anapoogea maji ya baridi huamsha T-receptor cells ambazo hupelekea msukumo wa homoni ya testosterone kutoka kwenye gonads na kukuweka katika hali ya kukabiliana na jambo (Beast mode).

Beast Mode huchochea silika zako za awali (primal insticts). na Testosteron ndio homoni ijulikanayo kama beast mode hormone.

Imeandikwa na SAMUEL MACHA
FIT BY WAYNE.

Simu: 0753068572/0676068572
Whatsapp: WHATSAPP

Reference:

The Obesity Code by Dr Jason Fung
The Diabetes Code by Dr Jason Fung
Why we get sick by Benjamin Bikman PhD
Semen retention miracle by Joseph H. Peterson

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed