Skip to main content

MAZOEA/TABIA 10 ZA KUJENGA UDHIBITI WA KUONDOKANA NA UNENE

 

Ulaji na mtindo mbaya wa maisha husababisha unene.

MAZOEA/TABIA 10 ZA KUJENGA UDHIBITI WA KUONDOKANA NA UNENE.

Unene kupita kiasi ni tatizo la kiafya ulimwenguni kote. Uzito uliopitiliza ni kuwa na 10% hadi 19% zaidi ya uzito sahihi unaotakiwa kiafya.

Wakati Unene kupita kiasi ni kuwa na zaidi ya 20% ya uzito sahihi unaotakiwa kadiri ya urefu, jinsia na ukubwa wa mifupa.

Kiini cha tatizo hili ni kiasi kikubwa cha Kalori. Uzito huongezeka pale ambapo unakula kalori nyingi zaidi kuliko mwili wako uwezavyo kutumia. Kalori za ziada huhifadhiwa kama mafuta mwilini. Kwa kila kalori 3,500 za ziada inayopokelewa mwilini, nusu kilo ya uzito huongezeka.

UZITO SAHIHI UNAOTAKIWA KUA NAO KULINGANA NA UREFU PAMOJA NA JINSIA.

jedwali la uzito sahihi kulingana na urefu pamoja na jinsia.

MAZOEA 10 YA KUJENGA UDHIBITI WA KUDUMU WA UZITO SAHIHI.

  1. Tumia vyakula vya mimea/nafaka ambazo hazijakobolewa, vyakula hivi hua na wingi wa nyuzinyuzi na viinilishe. (Ili kujua madhara ya nafaka zilizokobolewa, soma HAPA (madhara ya nafaka zilizokobolewa) 
  2. Usiache kula kifungua kinywa kwa kutumia chakula chenye mchanganyiko wa nafaka mbali mbali pamoja na matunda.
  3. Tumia milo miwili au mitatu kwa siku katika nyakati maalum bila kula kitu chochote katikati ya milo.
  4. Kula chakula chako au tafuna taratibu, tumia muda kufurahia chakula chako, hii itasaidia chakula chako kusagwa vizuri tumboni.
  5. Kula matunda katika kukamilisha mlo wako badala ya kutumia vitu vya sukari kama vile soda au juisi.
  6. Usile chakula chako cha jioni/usiku kwa kuchelewa. (weka tabia ya kutokula zaidi ya saa 2 au 3 usiku, na usitumie vyakula vya wanga wakati wa usiku)
  7. Kunywa maji mengi badala ya kunywa juisi au soda.
  8. Fanya mazoezi kila siku walau kwa dakika 30 au tembea Hatua 10,000 kwa siku. 
  9. Epuka vitu vyenye madhara kama vile pombe, tumbaku (sigara), kafeni, dawa za kulevya n.k)
  10. Fanya kitu chenye manufaa kama vile kusoma vitabu, kucheza na watoto, kutembea nk badala ya kukaa na kuangalia TV au kukaa tu na kula.

Kama ukiweza kuwa na tabia 10 zilizotajwa hapo juu na ukiweza kuzifanya sehemu ya maisha yako, basi tatizo la uzito uliopitiliza/unene litaondoka kwenye maisha yako.

Watu wengi hua wanatamani kuondokana na unene, lakini unapowaambia mambo ya kufanya ili waondokane na unene, hawafanyi. Hua wanataka kupungua kwa miujiza, sasa hamna miujiza katika kupunguza unene, ni lazima kufwata kanuni za kua na afya bora.

Hua napenda kusema ya kwamba, ROMA HAIKUJENGWA KWA SIKU MOJA. Hukua mnene ndani ya siku moja, bali ni siku nyingi, Hivyo usitafute njia za mkato, hazitakusaidia kwa muda mrefu.

kwa msaada zaidi juu ya Kupunguza na kuondokana na  unene.
SIMU: 0753068572/0676068572
WHATSAPP: 0621068072  au Bonyeza WHATSAPP

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed