Skip to main content

MADHARA YA KUTUMIA MKATE MWEUPE (NGANO ILIYOKOBOLEWA)

 

Mkate Mweupe uliotengenezwa kwa ngano iliyokobolewa

MADHARA YA KUTUMIA MKATE MWEUPE (NGANO ILIYOKOBOLEWA)

Ngano ni moja wapo ya nafaka zinazotumika zaidi duniani. Ngano inashika namba 2, namba moja ikiwa ni mahindi na namba 3 ikiwa ni mchele kwa matumizi duniani. 

Kuna mikate ya aina mbali mbali, na asilimia kubwa ya mikate hutengenezwa kwa kutumia Unga wa Ngano. kuna aina 2 za unga wa Ngano, 

  1. Unga wa Atta. (Unga wa Ngano ambao haujakobolewa)
  2. Unga wa Ngano uliokobolewa. (ngano nyeupe)
Unga wa Ngano mweupe (uliokobolewa) ndio unaongoza kwa kutengeza mikate kwa asilimia kubwa. Ila madhara ya kutumia unga wa ngano uliokobolewa ni makubwa kuliko ambavyo watu wanafahamu.

NINI MADHARA YA KUTUMIA NAFAKA ZILIZOKOBOLEWA?

Kwa kawaida, mtu huchukua takribani dakika 5 kuweza kula kipande cha mkate wa unga wa Atta. (yaani mkate wa unga wa Ngano ambao haujakobolewa). Lakini mtu hutumia sekunde chache kuweza kula kipande cha mkate wa unga wa Ngano iliyokobolewa. (unga mweupe wa ngano).

Daktari anayefahamika kwa jina la Don Colbert aliwahi kusema "The whiter the bread, the sooner you are dead". Ikiwa na maana ya kwamba, kadiri unavyotumia Mkate mweupe (ngano iliyokobolewa), ndivyo unavyozidi kupunguza siku zako za kuishi.

Utumiaji wa nafaka zilizokobolewa ndio chanzo kikubwa cha Unene, kisukari, Magonjwa ya moyo, Saratani pamoja na magonjwa mengine mengi yasioambukiza.

KWA NINI MKATE MWEUPE (NGANO ILIYOKOBOLEWA NI MBAYA)

  • Ngano iliyokobolewa hupoteza thamani yake ya lishe. (nutritional Value). Hii hupelekea kua na kiwango kikubwa cha sukari ambayo mwilini huhifadhiwa kama mafuta.
  • Nyuzinyuzi (fiber) pamoja na Viini vyake huondolewa na kubakisha wanga (starch) peke yake
  • Wanga (starch) hua oxidized, kuongezewa hydrogen (hydrogenation) pamoja na sukari ya ziada na hivyo kuifanya iwe na Glycemic Index ya juu sana. (Glycemic Index ni kiwango cha jinsi wanga unavyogeuzwa kua sukari mwilini na kuhifadhiwa kama mafuta badala ya kuchomwa kama nishati)
  • Hufanyiwa Bleaching, kiasi kidogo cha chloride inaweza kugeuzwa na kua kemikali ambayo huongeza uwezekano wa kupata ugonjwa wa kisukari.

NINI CHA KUFANYA KUONDOKANA NA MADHARA HAYA?

Jambo kuu la kufanya ni kuachana na vyakula vitokanavyo na nafaka zilizokobolewa. Mfano Wali mweupe, tambi, sembe, Vyakula vya ngano iliyokobolewa kama vile chapati, maandazi, sambusa, kalmati, visheti, N.K

Badala yake ni vyema kutumia zaidi vyakula vya nafaka ambayo haijakobolewa kama vile dona, wali wa kahawia (wali wa brown), Unga wa Atta (ngano ambayo haijakobolewa) na nafaka nyinginezo ambazo hazijakobolewa.

Kujitahidi kutumia formula ya sahani ya mlo unaofaa. kama ambavyo inaelezewa katika makala hii. Bonyeza HAPA (Sahani ya Mlo Unaofaa)

Kufanya mazoezi walau mara 3 kwa wiki. Hakikisha unafanya mwili unakua active ili uweze kutumia na kuchoma mafuta kama nishati. Unaposhindwa kutumia wanga kama nishati, hugeuzwa na kuhifadhiwa kama mafuta mwilini. Na sio lazima kufanya mazoezi makali, ila unaweza kufanya mazoezi mepesi yanayoendana na mwili au uwezo wako, kushuka kituo kimoja kabla ya kituo husika ili ikupe nafasi ya kutembea, kutumia ngazi badala ya lift, kutembea kwa walau dakika 20 kwa siku N,K.

Kunywa maji ya kutosha kila siku kulingana na uzito wa mwili wako. kwa kawaida, katika kila kilo 20 za mwili wako, unatakiwa kunywa lita moja za maji. Mfano mtu mwenye kilo 80, kuna 20 mara 4 ndani yake. Hivyo atatakiwa kunywa walau lita 4 kwa siku ikiwa ni kiwango cha chini.

FAIDA ZA KUTUMIA NAFAKA AMBAZO HAZIJAKOBOLEWA.

  • Zina wingi wa thamani ya lishe (nutritional value)
  • Zina vipengele vyote muhimu kwa ajili ya kurutubisha mwili. (entire grain, kernel, bran na germ of endosperm). [zilizokobolewa hua na endosperm peke yake]
  • Zina wingi wa nyuzinyuzi (dietary fiber)
  • Zina wingi wa anti oxidants
  • Zina wingi wa Protini inayoleta amino acid ya lysine
  • Zina wingi wa madini kama vile magnesium, manganese, phosphorus pamoja na selenium
  • Zina vitamini muhimu kama vile niacin, Vitamin B6 pamoja na Vitamin E.

UMUHIMU WA NYUZINYUZI (DIETARY FIBER)

  • Husaidia kupunguza matatizo yatokanayo ya mmeng`enyo wa chakula kama vile kukosa choo na bawasiri.
  • Husaidia kuondokana na matatizo ya magonjwa ya moyo.
  • Husaidia kuondokana na matatizo ya kisukari.
  • Husaidia kuweza kuondokana na changamoto ya unene uliopitiliza na kua na uzito sahihi.
Imeandikwa na Samuel Macha, 
FIT BY WAYNE.

Kwa msaada zaidi:

simu: 0753068572
Whatsapp: 0621068072

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed