Skip to main content

JINSI YA KUZUIA NA KUKABILIANA NA TATIZO LA VIMBE KWENYE KIZAZI (FIBROIDS)

 

JINSI MWANAMKE ANAVYOWEZA KUZUIA AU KUKABILIANA NA VIMBE KWENYE KIZAZI (FIBROIDS).

Fibroids ama vimbe kwenye kizazi ni tatizo la kihomoni ambalo linatokea kwa mwanamke ambae yupo katika umri wake anaoweza kuzaa.

Hii humaanisha ya kwamba fibroids hua zinalishwa na homoni ya oestrogen. Fibroids ni kama magugu ambayo huota shambani katika shamba ambalo halifanyiwi palizi au limeachwa.

Wanawake walio katika hatari ya kupata fibroids ni;-

ยท       Wanawake wenye umri kuanzia miaka 28, japokua hata chini ya miaka 28 wanaweza kupata.

ยท       Wanawake wanene.

ยท       Wanawake weusi (waafrika); hii ni kwa sababu ya ulaji pamoja na mtindo wa maisha.

ยท       Wanawake wenye shida ya presha pamoja na kisukari.

ยท       Historia ya familia kua na fibroids. Familia huambukizana epigenetics na endocrine disruptors kutokana na tabia ya ulaji na mtindo wa maisha ya familia husika.

ยท       Wanawake ambao hawajazaa. Haswa ambao wamefika miaka 30.

ยท       Wanawake wenye upungudu wa Vitamin D.

ยท       Wanawake wenye ulaji mbovu mfano matumizi ya sukari, nafaka zilizokobolewa, mafuta ya mbegu pamoja na vyakula vilivyochakatwa.

ยท       Matumizi ya soya, maziwa yaliyochakatwa

ยท       Pombe kwa sababu ni oestrogenic.

DALILI ZA MWANAMKE MWENYE FIBROIDS.

ยท       Kutokwa na damu nyingi sana wakati wa hedhi.

ยท       Kutokwa na damu katikati ya hedhi na hedhi nyingine (yaani siku ambazo sio za hedhi)

ยท       Maumivu makali wakati wa hedhi.

ยท       Kupata kitambi cha chini ambacho ni kigumu kupungua.

ยท       Kushindwa kubeba ujauzio kwa sababu fibroids zinazuia kutungwa kwa mimba.

ยท       Mimba kutoka mara kwa mara.

NJIA RAHISI ZA KUPONA VIMBE KWENYE KIZAZI (FIBROIDS)

ยท       Kuacha matumizi ya sukari pamoja na nafaka zilizokobolewa

ยท       Kuacha matumizi ya mafuta ya mbegu

ยท       Kufunga kula mara kwa mara/ kila siku

ยท       Kuacha matumizi ya ngano

ยท       Kutembea juani wakati wa asubuhi

ยท       Kuacha matumizi ya pombe na sigara

ยท       Kupunguza uzito kama ni mnene

ยท       Kupumzika na kulala walau saa 8 kwa siku.

ยท       Kufanya mazoezi walau mara 3 kwa wiki

Kitu kikubwa kinachotishia afya ya uzazi ni vitu vinavyochochea na kusababisha uharibufu au mvurugiko wa homoni za mwanadamu.

Kabla ya mwanamke yoyote yule kukubali kufanyiwa upasuaji kwa ajili ya vimbe kwenye kizazi (fibroids) ni vyema kwanza akabadilisha ulaji wake pamoja na mtindo wa maisha.

Endapo utafanya upasuaji na huku vile visababishi vikuu bado havijaondolewa, maana yake zitaturi tena katika maisha yako.

Reference: www.amerix.co.ke


Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...