Skip to main content

JINSI YA KUZUIA NA KUKABILIANA NA TATIZO LA VIMBE KWENYE KIZAZI (FIBROIDS)

 

JINSI MWANAMKE ANAVYOWEZA KUZUIA AU KUKABILIANA NA VIMBE KWENYE KIZAZI (FIBROIDS).

Fibroids ama vimbe kwenye kizazi ni tatizo la kihomoni ambalo linatokea kwa mwanamke ambae yupo katika umri wake anaoweza kuzaa.

Hii humaanisha ya kwamba fibroids hua zinalishwa na homoni ya oestrogen. Fibroids ni kama magugu ambayo huota shambani katika shamba ambalo halifanyiwi palizi au limeachwa.

Wanawake walio katika hatari ya kupata fibroids ni;-

·       Wanawake wenye umri kuanzia miaka 28, japokua hata chini ya miaka 28 wanaweza kupata.

·       Wanawake wanene.

·       Wanawake weusi (waafrika); hii ni kwa sababu ya ulaji pamoja na mtindo wa maisha.

·       Wanawake wenye shida ya presha pamoja na kisukari.

·       Historia ya familia kua na fibroids. Familia huambukizana epigenetics na endocrine disruptors kutokana na tabia ya ulaji na mtindo wa maisha ya familia husika.

·       Wanawake ambao hawajazaa. Haswa ambao wamefika miaka 30.

·       Wanawake wenye upungudu wa Vitamin D.

·       Wanawake wenye ulaji mbovu mfano matumizi ya sukari, nafaka zilizokobolewa, mafuta ya mbegu pamoja na vyakula vilivyochakatwa.

·       Matumizi ya soya, maziwa yaliyochakatwa

·       Pombe kwa sababu ni oestrogenic.

DALILI ZA MWANAMKE MWENYE FIBROIDS.

·       Kutokwa na damu nyingi sana wakati wa hedhi.

·       Kutokwa na damu katikati ya hedhi na hedhi nyingine (yaani siku ambazo sio za hedhi)

·       Maumivu makali wakati wa hedhi.

·       Kupata kitambi cha chini ambacho ni kigumu kupungua.

·       Kushindwa kubeba ujauzio kwa sababu fibroids zinazuia kutungwa kwa mimba.

·       Mimba kutoka mara kwa mara.

NJIA RAHISI ZA KUPONA VIMBE KWENYE KIZAZI (FIBROIDS)

·       Kuacha matumizi ya sukari pamoja na nafaka zilizokobolewa

·       Kuacha matumizi ya mafuta ya mbegu

·       Kufunga kula mara kwa mara/ kila siku

·       Kuacha matumizi ya ngano

·       Kutembea juani wakati wa asubuhi

·       Kuacha matumizi ya pombe na sigara

·       Kupunguza uzito kama ni mnene

·       Kupumzika na kulala walau saa 8 kwa siku.

·       Kufanya mazoezi walau mara 3 kwa wiki

Kitu kikubwa kinachotishia afya ya uzazi ni vitu vinavyochochea na kusababisha uharibufu au mvurugiko wa homoni za mwanadamu.

Kabla ya mwanamke yoyote yule kukubali kufanyiwa upasuaji kwa ajili ya vimbe kwenye kizazi (fibroids) ni vyema kwanza akabadilisha ulaji wake pamoja na mtindo wa maisha.

Endapo utafanya upasuaji na huku vile visababishi vikuu bado havijaondolewa, maana yake zitaturi tena katika maisha yako.

Reference: www.amerix.co.ke


Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed