Skip to main content

MBINU 3 ZA MAMA ANAYENYONYESHA KUPATA MAZIWA MENGI

 

ILI MWANAMKE AZALISHE MAZIWA MENGI

Kwa muda mrefu sana wanawake wanaonyonyesha wamekua wakiambiwa mambo kadhaa ili kuweza kuzalisha maziwa ya kutosha kwa ajili ya watoto wao.

Mfano wa vitu wanavyoambiwa ni;

ยท       Kula mara kwa mara upate maziwa

ยท       Kunywa maziwa ili upate maziwa

ยท       Kunywa soda ya coca ili uzalishe maziwa

ยท       Kula matunda mengi

ยท       Kunywa juisi ya Ribena

ยท       Na mengine mengi.

Maziwa ya mama huzalishwa katika FAT LOBULES. Na ndio sababu kwa nini matiti ya mama hua makubwa pale anapokua mjamzito.

Hakuna bomba kwenye titi la mwanamke ambalo litazalisha maziwa eti kwa sababu amekula chakula flani. Chakula anachokula mama ni lazima kipitie mmeng`enyo na kuweza kufyonzwa katika mwili.

Maziwa ya mama huhifadhiwa katika Fat Lobules kabla ya kusisimuliwa ili yatoke katika chuchu.

Vyakula pekee amavyo mama anahitaji ni;

ยท       Nyama

ยท       Mayai (ya kienyeji)

ยท       Samaki

ยท       Shahamu muhimu (essential fats) kama vile mafuta ya wanyama, nazi na parachichi.

Mama anatakiwa kuzingatia kumnyonyesha mtoto mara kwa mara ili kuweza kusisimua uzalishwaji wa maziwa.

Ni lazima mama afwate kanuni ya PQRSTU kwa ajili ya kuzalisha maziwa ya  kutosha kwa mtoto.

ยท       POSITION: mkao wa mtoto wakati ananyonya

ยท       QUALITY: ubora wa chakula ambacho amma anakula, ni lazima kiwe chenye thamani kubwa ya lishe.

ยท       REGULARITY: mama anamnyonyesha mtoto mara ngapi kwa siku?

ยท       SLEEP: mama anatakiwa ajitahidi kupata usingizi na kupumzika pale anapopata nafasi.

ยท       UNINTERRUPTED BREAST FEEDING TIME: mama anatakiwa kumnyonyesha mtoto bila kukatishakatisha.

Bila kuzingatia kanuni hizi, mama hawezi kupata maziwa ya kutosha kwa ajili ya mtoto.

Kama ni mama unanyonyesha, wasiliniana nami uweze kupata mwongozo wa mama anayenyonyesha. Bonyeza HAPA kisha unitumie ujumbe mfupi.

Reference; www.amerix.co.ke

 


Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...