Skip to main content

FUNGA KULA ILI KUEPUKANA NA MARADHI

 

FUNGA KULA ILI UEPUKANE NA MARADHI.



Mwili wa mwanadamu haukuumbwa ili uwe na maradhi au kuugua. Lakini ni kwa nini mwanadamu hua anasumbuliwa na maradhi?

Jaribu kuangalia wanyama kama sokwe, papa au mbwa mwitu. Ni wanyama ambao ni nadra kuona wanaugua. Lakini umeshawahi kujiuliza ni kwa nini?

Jarbu kuangalia mazingira ya ulaji unaokuzunguka. Karibia kila kitu unachokula hakifai katika mwili wako lakini bado unakula. Wanadamu wanakula PRODUCTS Zaidi kuliko wanavyokula CHAKULA. Products ni vitu ambavyo miili yetu haiwezi kumeng`enya vinapofika tumboni. Na ndio maana mwanadamu anazungukwa na maradhi katika maisha yake.

Ipo mbinu moja ya kale sana ambayo mwanadamu yoyote yule akiwa anaitumia hatakua mtu anayepata maradhi au kuugua ugonjwa wa aina yoyote ule. Mbinu hiyo si nyingine bali KUFUNGA KULA (FASTING)

Unapokua umezuia mwili wako kula chakula kwa walau muda wa masaa 16 na Zaidi, mwili wako utakua katika hali ijulikanayo kama AUTOPHAGY. Yaani mwili wako hautafuni chakula, ila unaaza kutafuna sehemu za seli ambazo ni mbaya na zingeweza kusababisha ugonjwa. Seli zako za mwili zinaanza kushambulia sehemu mbaya za seli ili kuweza kuzitumia kama nishati badala ya kuruhusu zisababishe madhara katika mwili.

Mwili wako ni mfumo ambao una akili sana, ila wewe ndio ambae ni mjinga kwa kuulisha takataka na kutokufunga. Mwili una akili kiasi kwamba unafahamu ni vitu gani vinatakiwa kuondolewa kwanza pale ambapo mtu anakua amefunga. Hii huruhusu kuzaliwa kwa seli mpya ambazo zina manufaa. (na ndio maana watu ambao hufunga kula mara kwa mara huchelewa kuzeeka ukilinganisha na watu ambao hua wanakula kila siku)

Unapofunga kula, mwili huachilia homoni ya kukua (growth hormone) ambayo itasaidia katika mchakato wa uponyaji.

Hivi ni vitu ambavyo hutaambiwa hospitali, lakini ndio siri ambazo wazee wa kale walitumia wakaishi muda mrefu pasipokua na maradhi.

na Samuel Macha 0753068572

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...