Skip to main content

UZITO HUPOTEA KIUNONI NA SIO KWENYE MZANI

 

UZITO/UNENE HUPOTEA KIUNONI NA SIO KWENYE MZANI.

Ukitaka kutambua mwenendo wako wa kupungua uzito au unene, basi tumia kiuno chako na wala usitumie mzani.

Mzani hauwezi kukupa ufanisi wa kujua uzito au unene ambao umepungua. Mzani hua unakupa tu uhakika, lakini kiuhalisia haikuonyeshi maendeleo yako kwa ufasaha.

Usitumie muda mwingi sana kuangalia mzani wako unasemaje, kwa sababu mizani tofauti hua na calibration ya tofauti na pia unapopima kwa nyakati tofauti hua unapata namba tofauti.

NJIA BORA YA KUJUA UZITO AU UNENE ULIOPUNGUA NI IPI?

Njia bora Zaidi ni WAIST-TO-HEIGHT RATIO (WSR). Lakini pia, kuna mambo kadhaa ambayo unaweza kuangalia na kujua ya kwamba unapata matokeo mazuri. Mfano wa njia hizo ni; -

ยท         Kupata usingizi mzuri ambao mwanzoni hukua unaupata.

ยท         Kutokupata njaa mara kwa mara na kushiba mapema hata kama umekula chakula kidogo au mara moja kwa siku (improved insulin sensitivity) ambapo hapo awali ulikua unakula sana na kupakua chakula kingi ili ushibe.

ยท         Presha ya chini (diastolic blood pressure) kusoma kiwango cha chini ukilinganisha na hapo awali.

ยท         Kupungua kwa mapigo ya moyo tofauti na mwanzo.

ยท         Uwezo mkubwa wa kufanya kazi kwa muda mrefu bila kujihisi mchovu.

ยท         Kutokupatwa na hasira mara kwa mara tofauti na mwanzo.

ยท         Na mengine mengi sana ambayo siwezi kuyataja yote.

Hivyo basi, ni vyema ukazingatia mabadiliko ya kiuno chako Zaidi kuliko kuangalia kilo zako kwenye mzani.

JINSI YA KUANGALIA KIWANGO CHA UNENE WAKO KUTUMIA WSR.

Kama wewe ni MWANAUME, basi kiuno chako kinatakiwa kuwakati ya inches 31 hadi 35. Na kwa MWANAMKE inatakiwa isizidi inches 36.

JINSI YA KUKOKOTOA WSR YAKO.

Pima mzunguko wa kiuno chako katika cm (sentimita), ugawanye kwa urefu wako kwa cm (sentimita).  

WSR= Waist (kiuno) cm รท Height (urefu) cm

Jibu utakalopata inatakiwa isizidi 0.5 kwa MWANAUME na MWANAMKE.

Mfano.

SAMUEL MACHA, Kiuno ni inches 31. Ambayo ni sawa na cm 78.7 na Urefu ni cm 175.

WSR= Waist (kiuno) cm รท Height (urefu) 

WSR= 78.7cm รท 175 cm = 0.4

Hivyo WSR ya SAMUEL MACHA ni 0.4

Na hivyo ndio jinsi ya kujua kama upo ndani ya unene unaotakiwa au la. Ila kikubwa ni PROGRESS OVER PERFECTION. Yaani huezi kua mkamilifu kwa siku moja, bali unatakiwa kuhakikisha ya kwamba kila siku unapiga hatua, na leo uhakikishe unakua bora kuliko jana. ROMA HAIKUJENGWA KWA SIKU MOJA.

Reference:

www.amerix.co.ke

 


Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...