Skip to main content

MAUMIVU YA KICHWA MARA KWA MARA

 

MAUMIVU YA KICHWA MARA KWA MARA.

Yawezekana hua unasumbuliwa au umeshaona mtu ambae hua anasumbuliwa na maumivu ya kichwa ya mara kwa mara.

Na mara nyingi maumivu haya hua hayaishi hata kama ukimeza paracetamol au dawa yoyote ya kutuliza maumivu.

Wengine huenda hospitali, kila vipimo wanavyofanyiwa huonyesha ya kwamba hawana shida yoyote ile. Mpaka wengine hudhania ya kwamba kuna mtu anawaloga.

NI KWA NINI MAUMIVU HAYA HUTOKEA?

Kisababishi kikuu hua ni upungufu wa madini ya Sodium mwilini. Kua na upungufu wa sodium kitaalam huitwa HYPONATRAEMIA.

Watu wenye upungufu wa Sodium hua na shida kwenye pampu ya umeme katika seli zao ijulikanayo kama Sodium-Potassium Channel Pump.

Pampu hii hutoa chaj za umeme kwa ajili ya kupeleka nguvu katika misuli na mfumo wa fahamu ili iweze kufanya kazi vizuri.

Kukiwa na shida katika pampu hiyo, hutoa potassium kwa wingi sana katika seli za ubongo na hivyo kusababisha hali ya excitation katika chaneli za fahamu na matokeo yake kupata maumivu ya kichwa.

Unapofanya shughuli za kutumia nguvu au akili na kuwaza sana, chaleni hiyo huleta voltage kubwa ya umeme inayoendeshwa na uwiano kati ya elektroliti za sodium pamoja na potassium.

Uwiano huu unapokosekana, pampu hiyo huanza kutoa elektroliti za potassium pasipo mpangilio maalum, na hivyo kusababisha maumivu ya kichwa.

JE, NINI CHA KUFANYA KUKABILIANA NA HILO?

Ni rahisi sana, tumia chumvi.

Chumvi itakupa Sodium ambayo itasaidia katika uwiano sawa wa chaneli ya pampu ya potassium.

        I.            Chukua chumvi kidogo katika vidole vyako kwa kufinya dole gumba pamoja na kidole cha kwanza. (pinch of salt). Au nusu kijiko cha chai na kisha uweke kwenye glass au kikombe cha maji ya vuguvugu.

      II.            Kunywa maji hayo kila asubuhi na kabla ya kwenda kulala usiku.

Kwa kufanya hivyo, utaondokana na tatizo la kuumwa kichwa mara kwa mara.

Okoa pesa zako kwa kumeza paracetamol kila siku.

Imeandikwa na SAMUEL MACHA, mwanzilishi wa FIT BY WAYNE

Reference:

www.amerix.co.ke


Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...