Skip to main content

MADHARA YA SODA KATIKA MWILI WAKO

 

MADHARA YA SODA KATIKA MWILI WAKO.

Moja ni moja kati ya vinywaji vinavyopendwa na kutumiwa sana na watu wengi. Na mbaya Zaidi, hata watoto ambao hawana hatia hupewa soda na wazazi wao kwa madai ya kuwaonyesha upendo kwa kuwaburudisha.

Lakini kitu ambacho hatukifahamu ni kwamba tunajichimbia makaburi wenyewe na kujiwekea nafasi ya kuumwa magonjwa ambayo yanatesa sana baadae na kuyatibu ni gharama kubwa sana.

Soda imetengenezwa na vitu vingi vyenye sumu ambavyo havina faida yoyote katika mwili wa mwanadamu, lakini mbaya Zaidi ni kwamba vina madhara makubwa ambayo hua hayatokei kwa haraka bali huja taratibu katika maisha ya mwanadamu.

KEMIKALI ZILIZOPO KATIKA CHUPA YA SODA NI; -

ยท         Carbonated water

ยท         High fructose corn syrup

ยท         Caramel

ยท         Phosphoric acid

ยท         Artificial flavouring

ยท         Caffeine.

Hivyo wakati wowote ule unapokunywa chupa ya coca cola, fikiria unaingiza vitu vyote hivyo katika mwili wako ndani ya dakika chache.

MADHARA YAKE; -

ยท         Kupata ini lenye mafuta (fatty liver)

ยท         Kuharibika kwa mazingira ya seli za mwili na matokeo yake kupelekea saratani.

ยท         Unene na uzito uliopitiliza.

ยท         Magonjwa ya tumbo (inflamed gut)

ยท         Madhara makubwa ya kimetaboliki kama vile kisukari, presha na matatizo ya mifupa.

ยท         Ukungu katika uwezo wa kufikiri. (unakua mzito kufanya maamuzi na kujiona mchovu mchovu)

ยท         Uraibu na kuharibika kwa dopamine katika ubongo wako.

Ukishajua madhara yote hayo, sitegemei kuona tena unafurahia kunywa soda. Unauwzo wa kusema NAOMBA MAJI kila mara unapoulizwa UTAKUNYWA SODA GANI? Kwani itakua ni bora Zaidi.

Na kama wewe umeshindwa kuacha soda kutokana na kudharau kwako, basi walau usiwape watoto wako ili waweze kua na maisha marefu bila kuteseka na magonjwa yasioambukiza.

FIT BY WAYNE.


Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...