Skip to main content

MADHARA YA SODA KATIKA MWILI WAKO

 

MADHARA YA SODA KATIKA MWILI WAKO.

Moja ni moja kati ya vinywaji vinavyopendwa na kutumiwa sana na watu wengi. Na mbaya Zaidi, hata watoto ambao hawana hatia hupewa soda na wazazi wao kwa madai ya kuwaonyesha upendo kwa kuwaburudisha.

Lakini kitu ambacho hatukifahamu ni kwamba tunajichimbia makaburi wenyewe na kujiwekea nafasi ya kuumwa magonjwa ambayo yanatesa sana baadae na kuyatibu ni gharama kubwa sana.

Soda imetengenezwa na vitu vingi vyenye sumu ambavyo havina faida yoyote katika mwili wa mwanadamu, lakini mbaya Zaidi ni kwamba vina madhara makubwa ambayo hua hayatokei kwa haraka bali huja taratibu katika maisha ya mwanadamu.

KEMIKALI ZILIZOPO KATIKA CHUPA YA SODA NI; -

·         Carbonated water

·         High fructose corn syrup

·         Caramel

·         Phosphoric acid

·         Artificial flavouring

·         Caffeine.

Hivyo wakati wowote ule unapokunywa chupa ya coca cola, fikiria unaingiza vitu vyote hivyo katika mwili wako ndani ya dakika chache.

MADHARA YAKE; -

·         Kupata ini lenye mafuta (fatty liver)

·         Kuharibika kwa mazingira ya seli za mwili na matokeo yake kupelekea saratani.

·         Unene na uzito uliopitiliza.

·         Magonjwa ya tumbo (inflamed gut)

·         Madhara makubwa ya kimetaboliki kama vile kisukari, presha na matatizo ya mifupa.

·         Ukungu katika uwezo wa kufikiri. (unakua mzito kufanya maamuzi na kujiona mchovu mchovu)

·         Uraibu na kuharibika kwa dopamine katika ubongo wako.

Ukishajua madhara yote hayo, sitegemei kuona tena unafurahia kunywa soda. Unauwzo wa kusema NAOMBA MAJI kila mara unapoulizwa UTAKUNYWA SODA GANI? Kwani itakua ni bora Zaidi.

Na kama wewe umeshindwa kuacha soda kutokana na kudharau kwako, basi walau usiwape watoto wako ili waweze kua na maisha marefu bila kuteseka na magonjwa yasioambukiza.

FIT BY WAYNE.


Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed