Skip to main content

MADHARA YA PAMPERS (DIAPERS) KWA MTOTO


 

MADHARA YA PAMPERS (DIAPERS) KWA WATOTO.

Kwa wale ambao ni wakongwe kidogo, yaani waliozaliwa miaka ya 90 kurudi nyuma, wengi hawakuvalishwa pampers na wazazi wao, bali walivalishwa nepi au vinginevyo.

Lakini miaka ya hivi karibuni na tunapoelekea, kila mtoto anavalishwa pampers kulingana na utandawazi unavyozidi.

Kadiri siku zinavyozidi kwenda, ndivyo ambavyo mwanadamu anazidi kua mbali na asili yake na kuingia kwenye usasa ambao hauna chochote cha asili. Kadiri mwanadamu anavyoacha asili yake, ndivyo ambavyo matatizo ya ki afya huzidi Zaidi na Zaidi.

Pampers za watoto zimetengenezwa na kemikali hatarishi ambazo huathiri afya ya mtoto ambae anakua. Kemikali hizo hufanya mambo yafuatayo; -

ยท         Huharibu ngozi ya mtoto na kusababisha mzio wa ngozi maeneo ya sehemu zake za siri.

ยท         Kemikali hizi hufyonzwa katika tishu za mwili na kusababisha shida katika kinga ya mwili wa mtoto anaeivaa pampers hiyo.

ยท         Kemikali hizi ni neurotoxic (husababisha shida katika mfumo wa fahamu). Hii hupelekea kuharibika kwa mfumo wa fahamu wa mtoto (neurological failure)

ยท         Kemikali hizi huharibu mfumo wa homoni wa mtoto, matokeo yake ni kuleta shida kama vile matiti kwa mtoto wa kiume, hips na matako makubwa kama ya mwanamke wakati ni jinsi ya ME. Kuharibika kwa mfumo wa hedhi na afya ya uzazi kwa ujumla kwa watoto wa kike na mengine mengi.

ยท         Kuchelewa kukua kwa maumbile ya mtoto wa kiume kutokana na kufungiwa ndani ya pampers kwa muda mrefu yenye kemikali.

Kuna muda kama wazazi tunapaswa kujiuliza, je, kitu ambacho kinauwezo wa kufyonza mkojo, ni salama kwa ngozi ya mtoto?

Yatupasa kukaa chini na kutafakari kwa kina. Kitu hakiozi endapo kitatupwa. Hakiliwi na bacteria endapo utakifukia ardhini, ni salama kwa mtoto? Ni hatari hata kwa mazingira yetu ya kawaida.

Usikubali mtoto wako kutumia pampers (diapers). Hua inasikitisha kuona mtoto ana umri wa mwaka 1 bado anavaa pampers. Hii ni ishara ya kwamba jamii yetu ina wazazi wavivu. Ni AIBU kubwa.

Kuanzia umri wa miezi 6, mtoto anatakiwa aachwe huru, na mara nyingine acheze bila nguo. Haswa kama ni mtoto wa kiume.

Dunia inavyoenda na wakati, sio lazima asili yetu kuisahau, sio kila maendeleo ni mazuri.

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...