Skip to main content

JE, MLO WA ASUBUHI (BREAKFAST) UNA FAIDA YOYOTE?

 

JE, MLO WA ASUBUHI UNA FAIDA YOYOTE?

MLO WA ASUBUHI HAUNA FAIDA YOYOTE KWAKO.

Bila shaka umeshawahi kusikia au kuambiwa ya kwamba mlo wa asubuhi ni mlo wa muhimu kuliko mlo wowote ule. Tena ukaambiwa maneno kama vile ‘Kula mlo wa asubuhi kama mfalme, mlo wa mchana kama mtoto wa mfalme na mlo wa jioni kama ombaomba/maskini’

Je, kuna ukweli wowote kuhusiana na hili? Jibu ni HAPANA. Mlo wa asubuhi ni mlo usio na maana au faida yoyote kwako kuliko mlo wowote ule.

NI KWA NINI MLO WA ASUBUHI HAUNA MAANA AU FAIDA YOYOTE KWAKO?

Inapofika saa kumi alfajiri, mwili wako huachilia kiwango cha juu cha homoni aina nne.

        I.            Glucagon

      II.            Adrenaline

    III.            Cortisol

    IV.            Growth hormone

Homoni hizi hupandisha kiwango chako cha sukari kwenye damu wakati wa alfajiri kupitia mfumo wa kibaiolojia ujulikanao kama DAWN PHENOMENON. (ndio mfumo ambao hufanya mwanaume au mtoto wa kiume awe amesimamisha uume wake wakati anapoamka asubuhi).

Kiwango cha sukari kwenye damu hupanda kwa ajili ya kuandaa mwili kuweza kupambana na siku husika.

Growth hormone huandaa misuli kwa ajili ya kukabiliana na mchana wa siku husika na Adrenaline huleta uchangamfu wa akili kwa ajili ya asubuhi.

Hali ya sukari kwenye damu kupanda itakua hivyo mpaka dakika chache baada ya mchana (saa sita) ambapo itaanza kushuka, mwili sasa utaanza kutumia njia nyingine ya kupata glucose kutoka kwenye misuli pamoja na Ini. Katika hatua hii, mwili utaanza kugeuza mafuta ambayo yamehifadhiwa kwenye Ini kua glucose.

Hivyo basi, wakati wa asubuhi huna haya ya kula, hamna faida yoyote kwako. Mwili wako hauna ujinga wowote. Mwili hua unajua jinsi ya kujiweka sawa, ni wewe mwenyewe ndie ambae unaupeleka ndivyo sivyo.

JARIBU HIVI.

Pima nguvu na uchangamfu wa mwili wako siku ukiwa umekula asubuhi na siku ambayo haukula asubuhi. Utagundua yafuatayo…

Siku ukila asubuhi, utakua ni mtu mwenye uchovu mwingi, na utakua unapata njaa kali sana kama ikifika mchana usipokula kwa wakati.

Siku usipokula asubuhi, unakua na utimamu wa akili, unakua na uchangamfu pamoja na nguvu nyingi. Na unakua na uwezo wa kukaa muda mrefu bila kula.

TABIA YA KULA ASUBUHI IMETOKEA WAPI?

Afrika hatukua na tabia ya kula asubuhi, tabia hii ililetwa na wazungu. Waafrika walikua wanakula tu pale ambapo jua limeshafika kati.

Tabia ya kula asubuhi iliundwa na kampuni zinazotengeneza Breakfast kama vile Kellogs, General mills pamoja na Nestle ili wauze nafaka zao kama vile corn flakes, Oats meal, wheetabix n.k

Ndio maana kuna msemo wazee wengi hupenda kutumia unaosema. HAKUNA MWANADAMU WA KAWAIDA ANATAKIWA KULA WAKATI KUKU WAMELALA.

Imeandikwa na SAMUEL MACHA

Mwanzilishi wa FIT BY WAYNE.

 


Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed