Skip to main content

FAIDA 10 UTAKAZOZIPATA UKIACHANA NA MLO WA ASUBUHI.

 FAIDA 10 UTAKAZOZIPATA UKIACHANA NA MLO WA ASUBUHI.


FAIDA 10 ZA KUTOKULA ASUBUHI.

1. UTIMAMU WA AKILI/ KUMBUKUMBU NZURI

Unapokula chakula cha asubuhi, unafanya domapine zako zimwagike bila sababu za msingi na hivyo kufanya uzito katika ufanyaji kazi wa ubongo wako.

Watu ambao hula mlo wa asubuhi hua wanapata uvivu na ufanisi wa kazi zao kwa siku husika hua mdogo kwa sababu ubongo unakua bize kutengeneza dopamine ambayo imemwagika (dysregulated dopamine) pamoja na kusimamia umeng`enywaji wa chakula.

2. ARI YENYE NGUVU (ENERGETIC SOUL)

Kila alfajiri kuanzia mida ya saa 10, mwili wako huachilia homoni zijulikanazo kama counter-regulatory hormones ambazo hukusaidia kukupa nguvu ya kuweza kupambana na siku husika.

Hata kama una kazi ngumu kwa asubuhi hiyo, mwili wako unaweza kukupatia nguvu inayojitosheleza wewe kufanya shuhuli zako pasipo shida yoyote.

Watu ambao hula asubuhi hupata kitu kijulikanacho kama sugar crash ambapo miili yao hua dhaifu kwa sababu inakua bize kuweka uwiano wa sukari ambayo hupanda ghafla baada ya kula.

Umeshawahi kujiuliza ni kwa nini watu ambao hula asubuhi hua ni wachovu sana inapofika mchana? Ni kwa sababu ya sugar crash ambayo wanaipata.

3. UWEZO MKUBWA WA KUDHIBITI HISIA ZAKO.

Unapokua hujala asubuhi, jambo la kwanza tayari umeshinda kizuizi cha kwanza, ambapo unakua umeweza kuzuia mtiririko wa neurochemicals usio na sababu katika ubongo wako.

Unakua na control na hamna kitu kinachoweza kukuteteresha. Kwa sababu unakua na akili iliyotulia.

4. INSULIN SENSITIVITY NZURI.

Kila mara unapokula chakula, unasababisha insulin kupanda (insulin spike). Na hii hua ni mbaya Zaidi wakati wa asubuhi kwa sababu mwili wako tayari umeshaachilia counter-regulatory hormones zake.

Hivyo basi, mwili hulazimika kumwaga homoni ya glucagon ili kuweza kuleta uwiano wa insulin.

Unapokua huli asubuhi, insulin yako hubaki katika kiwango kidogo na hivyo afya yako inabaki kua imara.

5. UWIANO MZURI WA KIWANGO CHA SUKARI.

Kwa kua huli asubuhi, insulin hubakia kwa kiwango kidogo katika damu. Glucose ambayo iliachiliwa na homoni ya glucagon alfajiri ya saa 10 inatumika ili kufanya shuhuli zako zote za asubuhi.

Iwe unatembea au kukimbia au unafanya mazoezi, glucose ambayo iliachiliwa inatosha kabisa kukufikisha mchana ukiwa na nguvu.

Endapo kukawa na upungufu wa glucose inayohitajika, basi mwili wako utaanza kuchukua nishati kutoka kwenye mafuta ambayo yamehifadhiwa mwilini katika mchakato ujulikanao kama GLUCONEOGENESIS.

Hivyo mlo wa asubuhi bado unabaki hauna maana, mwili wako sio mjinga.

6. KUZALIWA KWA HOMONI YA TESTOSTERON.

Mwili pia huachilia homoni ya Growth Hormone ambayo huchochea kuzalishwa kwa testosterone.

Endapo utafanya mazoezi wakati wa asubuhi, kiwango chako cha testosterone kitapanda, ndio maana ndani ya nusu saa baada ya mazoezi ya asubuhi utaona unasimamisha sana uume (kwa wanaume).

Testosterone ni hormone ya kiume, unaweza kupata picha ni kwa nini wanaume ambao hawali asubuhi hua na nidhamu kubwa na nguvu Zaidi ukilinganisha na wanaokula asubuhi.

7. UIMARA WA KINGA YA MWILI.

Homoni za cortisole pamoja na adrenaline ambazo huzalishwa alfajiri hua ni anti-inflammatory. Husaidia chembechembe nyeupe za damu kupambana na inflammation kwa kuzuia njia za inflammation kutokea.

Ndio maana kwa wale wagonjwa, endapo wasipokula asubuhi na kula mchana, hupata nafuu kubwa ukilinganisha na siku ambazo wanakula asubuhi.

8. UIMARA WA AFYA YA TUMBO.

Endapo usipojaza tumbo lako na chakula, maana yake unatoa nafasi kwa tumbo lako kufanya regeneration na kupona, hivyo kua na afya imara Zaidi. (kumbuka afya ya mwili huanzia tumboni).

Hii hupelekea kuzalishwa kwa tindikali ya HCL, enzymes, gut microbiome, nyongo yenye afya, ini lenye afya pamoja na kibofu chenye afya.

9. KUONDOKANA NA NJAA KALI ZA MARA KWA MARA.

Umeshajiuliza ni kwa nini watu ambao hula asubuhi hua ni wachovu sana inapofika mida ya mchana? Na ambao hawakula asubuhi hufika mchana wakiwa na nguvu na wanakua wachangamfu (active).

Ni kwa sababu hupatwa na uraibu wa sukari. Miili yako inakua inawaomba sukari muda wote. Na kama kuna duka karibu, hua wanashindwa kujizuia na ni lazima wale au wanywe kitu cha sukari.

Hivyo kwa maelezo hayo machache, nina Imani utakua umejifunza moja kati ya vitu muhimu sana katika maisha yako.

Hamna anaekulazimisha kuyafwata haya. Ila tukumbuke ya kwamba matibabu hua ni gharama sana. Na matatizo mengi tunaweza kuyaepuka kabla hayajatokea au kabla hayajawa makubwa.

Imeandikwa na FIT BY WAYNE.

Reference: www.amerix.co.ke  

 

 

 


Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...