Skip to main content

MADHARA YA UNENE KWA WANAWAKE

 

MADHARA YA UNENE KWA WANAWAKE.

Wanawake hupata madhara makubwa Zaidi kwa sababu ya unene ukilinganisha na wanaume. Ingawa ifahamike ya kwamba, unene una madhara na athari kubwa wa mtu yoyote bila kujali ni wa jinsia gani.

NI KWA NINI MWANAMKE ANA ATHIRIKA ZAIDI?

ยท         MATATIZO YA UZAZI: wanawake wanene huwa wanakumbwa na changamoto nyingi za uzazi kutokana na kuvurugika kwa homoni pamoja na mzunguko wa hedhi.

ยท         KUPUNGUA KWA HAMU YA TENDO LA NDOA: mara nyingi huwalaumu wanaume kwamba wana uume mdogo au wanamwaga mapema. Lakini uhalisia ni kwamba wanawake wanene hua hawana hamu ya tendo la ndoa, ni ngumu kuamsha hisia zao za mahaba ukilinganisha na wanawake wenye uzito sahihi.

ยท         MATATIZO KATIKA KUJIFUNGUA: hua wanapoteza nguvu katika kusukuma mtoto wakati wa kujifungua. Au pia hua na watoto wakubwa (macrosomia) kutokana na athari za insulin kwa mtoto anaekua tumboni.

ยท         VISIRANI NA HASIRA ZISIZOKUA NA SABABU: wanawake wanene hua na self-esteem ndogo. (hali hafifu ya kujithamini). Hivyo wengi hua na visirani na hasira za hapa na pale bila sababu za msingi.

ยท         HUZUNI: mwanamke hujivunia uzuri wake na uzazi, mara nyingi anapokua mnene hujiona kama thamani yake ya uzuri imeshuka na huhisi ya kwamba mume wake au mwanaume yoyote hamuangalii kwa matamanio kama ilivyo kwa mwanamke mwembamba au mwenye uzito wa kawaida..

ยท         MAGONJWA YA AUTOIMMUNE: hua na hatari kubwa ya kupata magonjwa ya auto immune kama vile lupus, shida za homoni (thyroid conditions) n.k

ยท         SYDNROME X: wanawake wanene wengi huishia kupata shida za kimetaboliki kama vile kisukari, presha, saratani ya matiti n.k

Kama wewe ni mwanamke, na kama una mke ambae ni mnene. Msaidie aweze kua na uzito sahihi. Mtie moyo, kua nguvu yake anapokata tamaa, muaminishe ya kwamba inawezekana kuondokana na unene. Ukiwa kama baba wa familia, wewe ndio kichwa kwa maana ya kiongozi. Anza kuongoza familia yako katika ulaji unaofaa. Usitoe pesa kununua visivyofaa, ukitaka familia ile vyakula vizuri, maana yake hakikisha vinavyokuwepo nyumbani ni vyakula sahihi na sio products.

Na wewe kama mwanamke, ni lazima ukubali ndani ya nafsi yako kuondokana na unene. Kaa mbali na wale mashoga au mashosti ambao watakukatisha tamaa. Sio lazima utangaze kama unataka kupungua, wewe fanya kimya kimya. Watu wataona tu matokeo yako. Na wewe mwenyewe afya yako itaimarika.

Wanawake hua na athari mbaya Zaidi za unene ukilinganisha na wanaume, ingawa madhara yatokanayo na unene yanampata kila mwanadamu.

Na FIT BY WAYNE.


Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...