Skip to main content

JE, MAJI YA MOTO HUSAIDIA KUPUNGUZA KITAMBI?

 

JE, MAJI YA MOTO HUSAIDIA KUPUNGUZA KITAMBI?

Bila shaka umeshawahi kuona watu ambao hunywa maji ya moto na limao kila asubuhi huku wakisema ya kwamba wanafanya hivyo ili kupunguza kitambi.

Cha ajabu ni kwamba watu hawa wanafanya hivi lakini hawafanyi mabadiliko yoyote juu ya vyakula wanavyokula au mtindo wa maisha.

Kwa kifupi ni kwamba, ukiona mtu anasema anakunywa maji ya moto kwa lengo la kupunguza kitambi, ujue ni mvivu wa kubadilisha mtindo wake wa maisha na anapenda njia za mkato. Ila ukweli ni kwamba, katika kupunguza unene na kuondokana na kitambi, hua hamna njia za mkato.

UKWELI KUHUSU MAJI YA MOTO

Maji ya moto hayayeyushi mafuta kama wengi wanavyodhani. Na pia hayana mchango wowote katika kuyeyusha mafuta yanayosababisha unene mwilini mwa mwanadamu.

Tindikali ya Hydrocloric tumboni ndio husaidia katika kumeng`enya chakula, lakini sio maji ya moto.

Mtu anayekunywa maji ya moto na anayekunywa maji ya baridi, wote wanakunywa maji. Na hamna kitu cha ziada kinachowatofautisha.

Mdomo wa mwanadamu utapooza maji ili yawe katika joto linalotakiwa kabla ya kumeza. Ndio maana hakuna mtu anayeweza kumeza maji ya moto sana au yabaridi sana. Ni lazima atayachezesha mdomoni kwa sekunde kadhaa ili kuyafanya yawe na joto linalotakiwa kabla ya kumeza.

Wengine hudhania ya kwamba kwa sababu wanatoka jasho wanapokunywa maji ya moto, basi ndio wanapoteza mafuta ya unene. Ukweli ni kwamba, unatokwa na jasho kwa sababu mwili wako unajipooza. Hii ni kutokana na mfumo wa kibaiolojia ujulikanao kama HOMEOSTASIS.

Maji ya moto hayana kirutubisho chochote wala calorie ya aina yoyote. Hayana amino acids, ni maji tu ya kawaida kama ilivyo maji ya baridi.

Hivyo hamna ukweli wowote kama maji ya moto yanapunguza kitambi. Mafuta ya unene hayayeyuki kwa moto kama wengi wanavyodhani.

Na FIT BY WAYNE

www.amerix.ke.com (Reference)


Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...