Skip to main content

BAWASIRI NA JINSI YA KUJITIBU UKIWA NYUMBANI.

 

BAWASIRI NA JINSI YA KUKABILIANA NAYO NYUMBANI.

Bawasiri ni sehemu katika njia ya haja kubwa mwishoni (rectum) au dalili ya tatizo lenyewe.



Mishipa ya fahamu ya Bawasiri (Haemorrhoidal Plexus): ni mfumo wa mishipa ya fahamu, mishipa ya damu, tishu pamoja na misuli laini.

Haemorroidal Plexus ni kama sehemu laini ambayo husaidia kudhibiti haja kubwa wakati wa haja kutokana na mgandamizo mkubwa unaokuepo katika tumbo.

Plexus hii pia huhakikisha ya kwamba njia ya haja kubwa (anus) hufunga vizuri wakati mtu amepumzika au ametulia

Kuna aina mbili za haemorroidal plexus.

        I.            Internal plexus

      II.            External plexus

External plexus (mishipa upande wa nje) zina mishipa wakati internal plexus haina mishipa ya fahamu. Hivyo external plexus (mishipa ya nje) hua na maumivu makali wakati ya ndani haina maumivu.



Mishipa hii (haemorroids) huleta dalili pale zinapotanuka, kuvimba au kutokezea kwa nje ya njia ya haja kubwa.

Mtu anapokua katika sababu za hatari mara nyingi hupelekea kuvimba kusiko kwa kawaida katika sehemu ya mishipa hiyo (plexus)

Na inapotokea mtu anapata haja kubwa, basi hupelekea kutokwa na damu ambayo ni nyekundu ambayo haijakolea (bright red)

Plexus hizo zikitokea kwa nje, hupelekea choo kua na ute ute ambao husababisha sehemu ya haja kubwa kuwasha mara kwa mara.

Kisababishi kikuu hakijulikani, ila kuna sababu za hatari (risk factors) ambazo huongeza mgandamizo katika eneo la plexus.

SABABU ZA HATARI ZA BAWASIRI

        I.            Kutumia nguvu au kujikamua wakati wa haja kubwa

      II.            Kukaa chooni kwenye choo cha kukaa kwa muda mrefu (haswa watu ambao hua wanaenda na simu za mkononi au kusoma vitabu wanapojisaidia)

    III.            Mimba

    IV.            Kufanya ngono kinyume na maumbile

      V.            Uzito uliopitiliza au unene

    VI.            Majeraha katika uti wa mgongo

  VII.            Lishe isiyo na nyuzinyuzi

VIII.            Misuli dhaifu ya njia ya haja kubwa

    IX.            Historia ya bawasiri katika familia.

ISHARA NA DALILI ZA BAWASIRI.



        I.            Maumivu wakati wa kukaa au wakati wa haja kubwa

      II.            Kuwashwa katika sehemu ya haja kubwa

    III.            Kupata damu katika choo au damu kuwepo katika toilet paper uliyoitumia.

    IV.            Uvimbe wenye maumivu katika sehemu ya njia ya haja kubwa.

Kutokwa damu wakati wa haja kubwa ni ishara kubwa Zaidi ya bawasiri.

Bawasiri inaweza kutibiwa ukiwa nyumbani kwako, ingawa inaweza isipone kabisa. Matibabu ya nyumbani yatakuondolea maumivu, uvimbe pamoja na inflammation.

Bawasiri ambayo inajirudia mara kwa mara huenda ikahitaji matibabu Zaidi hospitali pamoja na upasuaji.

Bawasiri inaweza kujirudia baada ya matibabu, hivyo ni rahisi kudhibiti na kuzuia kuliko kuitibu na kupona.

JINSI YA KUJITIBU BAWASIRI NYUMBANI.

        I.            Unaweza kuloweka sehemu yako ya haja kubwa katika maji ya vuguvugu kwa dakika 15, hii itakusaidia kukupa unafuu.

      II.            Unaweza kutumia vilainisha choo ambazo husaidia kupata choo kilaini.

    III.            Sehemu ya njia ya haja kubwa inapaswa kuwa safi mara zote

    IV.            Unaweza kutumia dawa za maumivu kama vile paracetamol (Panadol) ili kupunguza maumivu.

Endapo kutokwa na damu kunaendelea ama hakuna nafuu yoyote, basi ni vyema kuonana na daktari kwa ajili ya matibabu Zaidi.

JINSI YA KUZUIA BAWASIRI.

        I.            Kula vyakula vyenye wingi wa nyuzi nyuzi kama vile wanga tata (complex carbohydrates) na mboga za majani pamoja na mbogamboga

      II.            Kunywa maji ya kutosha kulingana na uzito wako. (kwa kawaida, katika kila kilo 20 huhitaji maji lita moja). Hivyo utaangalia katika uzito wako, ishirini zipo ngapi.

    III.            Usijikamue au kulazimisha kupata haja. Nenda chooni pale unapohisi haja, kama huna haja, epuka kukaa chooni.

    IV.            Tumia choo cha kuchuchumaa badala ya kukaa.

      V.            Fanya mazoezi walau mara 4 kwa wiki. Ni muhimu sana.

    VI.            Punguza uzito kama ni mnene.

FANYA MAMBO YAFUATAYO KAMA HUA UNAPAMBANA NA BAWASIRI

        I.            Acha kabisa kutumia choo cha kukaa na uanze kuchuchumaa.

      II.            Usitumie maziwa pamoja na ngano. (lactose iliyopo kwenye maziwa hupelekea inflammation ya tumbo)

    III.            Acha kabisa matumizi ya sukari pamoja na asali (hii itasaidia Ini lako kua huru na kutengeneza chumvi za bile (bile salts) pamoja na lehemu (cholesterol)

    IV.            Usitumie mafuta ya mbegu (vegetable oils and seed oils). Hua yanaleta inflammation

      V.            Jifunze kufunga kula mara kwa mara. (mfumo wa OMAD au One Meal a Day ni njia nzuri Zaidi ili kuruhusu tumbo kua tupu na kujifanyia uponyaji)

    VI.            Epuka matumizi ya pombe. Huleta inflammation ya tumbo

hhhh

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...