Skip to main content

Madhara 7 Yanayowapata Wanawake Wanene

 

Madhara 7 Yanayowapata Wanawake Wanene.

Unene au uzito uliopitiliza una madhara kwa jinsia zote mbili, wanaume na wanawake, Ingawa kwa wanawake hupata madhara makubwa zaidi ukilinganisha na wanaume.

Madhara Yanayowapata Wanawake Wanene.

1. Kushindwa Kubeba Ujauzito

Wanawake wanene hupata changamoto nyingi zinazoathiri kizazi kama vile Polycistic Ovarian Syndrom ijulikanayo kama PCOS, Mji wa mimba kuzungungwa na mafuta au kuvurugika kwa hedhi inayosababishwa na kuvurugika kwa homoni.

2. Kupata Shida Wakati Wa Kujifungua

Wengi hupata tabu katika kusukuma mtoto au mtoto kua mkubwa (macrosomia). Hii husababishwa na uchochezi wa insulini kwa kiumbe kinachokua tumboni mwa mama kutokana na ulaji mbovu wa mama kwa muda mrefu.

3. Neuroticism (kutokua sawa kisaikolojia)

Mara nyingi hawa huwa na hasira za mara kwa mara, kujiona hawana thamani, kukosa kujiamini, kua na hisia hasi wakati mwingi, kua na ugomvi n.k. Hua wanajihisi kama vile kila mtu anawaona ni wabaya kutokana na miili yao ilivyo.

4. Sonona (Dpression)

Thamani ya mwanamke hua katika uzuri wake, tabia pamoja na Uzazi (kua mama), ndivyo jamii inavyowachukulia. Inapotokea amekua na uzito mkubwa, hukumbwa na msongo wa mawazo na kupelekea kua na sonona.

5. Magonjwa ya Kingamwili (Autoimmune)

Wanawake wanene wapo hatarini kupata magonjwa kama vile Lupus Disease (ni ugonjwa ambao mwili hushambulia viungo vya mwili),  magonjwa ya ngozi, matatizo ya homoni n.k.

6. Magonjwa ya Kimetaboliki

Kama vile kisukari, shinikizo la juu la damu (presha), saratani  ya matiti n.k

7. kupungua kwa Hamu ya Tendo la Ndoa

Hii huwapata wanawake wengi wanene, na matokeo yake wengi huwalaumu wanaume ya kwamba wana Uume mdogo, wanawahi kumwaga na wengi wao hudanganya ya kwamba wanafika kileleni, ila ukweli ni kwamba wengi hua hawafurahii Tendo hilo.

NB: Hamna unene wa kurithi, ila kuna kurithi mtindo mbaya wa maisha na mlo mbovu. Epuka Unene kwa nguvu zako zote, Chagua Afya, Chagua maisha.

Reference: Amerix


Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed