Skip to main content

Posts

Showing posts from February, 2022

Umuhimu Wa Kufunga Kula na Jinsi ya Kufunga Ipasavyo

  Kufunga Kula Kuna Faida Gani? Kufunga kula kulianza tangu enzi za kale. Hata wanadamu walioshi miaka mingi iliyopita walifunga kwa sababu mbali mbali. Hivi ni nani ambae alisema ya kwamba mwanadamu anatakiwa kula mara tatu kwa siku? Umeshawahi kujiuliza swali hilo? Je, kuna sababu za msingi zinazomfanya mwanadamu ale mara tatu kwa siku, na kuna faida gani endapo atakula pungufu ya hapo? Wagiriki wa kale waliamini ya kwamba kufunga huongeza uwezo wa utambuzi (cognitive ability). Wanafalsafa wengi waliamini ya kwamba kufunga kula ni moja wapo ya tiba katika mwili. Hippocrates ambae ni Baba wa Tiba (father of medicine) aliwaagiza wagonjwa wake wafunge kula ikiwa njia ya kwanza ya tiba kwao kabla ya kuwapa dawa yoyote ile. Hippocrates alisema " To eat when you are sick is to feed your illness" ikiwa na maana ya kwamba " kula chakula wakati ni mgonjwa ni sawa na kuulisha ugonjwa" Mwanafalsafa aitwaye Plutarch pia alisema " Instead of using medicine, better fast

Kati ya Nyama Inayofuatwa na Nzi, Au Isiyofuatwa na Nzi, Ununue Ipi?

  Nyama Inayofuatwa na Nzi Au Isiyofuatwa na Nzi. Ununue Ipi? karibia kila mtu ameshawahi au hua ananunua nyama Buchani au sehemu nyingine yoyote kwa ajili ya matumizi ya kula. Lakini kuna sehemu au Bucha ambazo nyama hufuatwa na nzi japokua bucha ni safi tu. Utaona tu kua muuza bucha anafukuza nzi mara kwa mara. Vilevile, kwenye bucha nyingi za kisasa pamoja na supermarkets, hua wananyama ambazo zinavutia sana machoni na ni safi, lakini hamna hata nzi mmoja anatua kwenye nyama hiyo, na hata akitua, basi hatathubutu kurudi tena. Je ni kwanini? Je, ununue Nyama Ipi? Kabla ya yote, USINUNUE NYAMA SUPERMARKET AU KWENYE BUCHA AMBAYO HAMNA NZI ANAYESOGEA. Ni kwa nini? Nyama hizi hutunzwa kwa kutumia Dutu (substance) hatarishi ijulikanayo kwa jina la Sodium Metabisulfite  Japokua taasisi nyingi duniani husema ya kwamba ni salama. Lakini jiulize... Je, ni salama kweli? kama wadudu kama nzi wanaikimbia, Je inafaa kwa matumizi ya mwanadamu? Mara nyingi wanyama au wadudu hua wanauwezo wa kutambu

Faida 8 Za Kutumia Majani Ya Nanaa (Mint Leaves)

  Faida Za Kutumia Majani ya Nanaa (Mint leaves). Majani ya nanaa hutumika kwa sababu mbali mbali duniani, wengi wakiwa wanatumia kama kiungo katika mapishi, dawa za meno hutumia majani haya kwa ajili ya kuleta harufu nzuri kwenye kinywa na kuzuia ukuaji wa bakteria kwenye meno na sababu nyingine nyingi. Zifuatazo ni faida zinazopatikana kwa kutumia majani ya Nanaa (mint) ki afya. Faida za Kutumia Majani ya Nanaa (Mint) 1. Hutibu Matatizo ya Tumbo Mint husaidia kutibu matatizo mbalimbali ya tumbo pamoja na kusaidia mmeng`enyo wa chakula na hivyo kuondokana na shida ya kukosa choo au kupata choo kigumu. 2. Hupandisha Kinga ya Mwili Kutokana na kua na wingi wa madini ya Phosphorus, calcium pamoja na Vitamin A,C,D na E ambazo huongeza kinga ya mwili kwa kulinda seli za mwili kutoka kwenye uharibifu. 3. Huondoa Chunusi Kwenye Ngozi Kutokana na tabia yake ya kua anti-inflammatory pamoja na anti-bacterial, majani ya nanaa husaidia kulainisha ngozi na kuondoa chunusi. Pia yana salicylic acid

Madhara 7 Yanayowapata Wanawake Wanene

  Madhara 7 Yanayowapata Wanawake Wanene. Unene au uzito uliopitiliza una madhara kwa jinsia zote mbili, wanaume na wanawake, Ingawa kwa wanawake hupata madhara makubwa zaidi ukilinganisha na wanaume. Madhara Yanayowapata Wanawake Wanene. 1. Kushindwa Kubeba Ujauzito Wanawake wanene hupata changamoto nyingi zinazoathiri kizazi kama vile Polycistic Ovarian Syndrom ijulikanayo kama PCOS, Mji wa mimba kuzungungwa na mafuta au kuvurugika kwa hedhi inayosababishwa na kuvurugika kwa homoni. 2. Kupata Shida Wakati Wa Kujifungua Wengi hupata tabu katika kusukuma mtoto au mtoto kua mkubwa (macrosomia). Hii husababishwa na uchochezi wa insulini kwa kiumbe kinachokua tumboni mwa mama kutokana na ulaji mbovu wa mama kwa muda mrefu. 3. Neuroticism (kutokua sawa kisaikolojia) Mara nyingi hawa huwa na hasira za mara kwa mara, kujiona hawana thamani, kukosa kujiamini, kua na hisia hasi wakati mwingi, kua na ugomvi n.k. Hua wanajihisi kama vile kila mtu anawaona ni wabaya kutokana na miili yao ilivyo.