Skip to main content

Vyakula 8 Vinavyosaidia Kusafisha Damu Kwa Asili

 

Vyakula 8 Vinavyosaidia Kusafisha Damu Kwa Asili.

Mara zote huwa tunavuta hewa, tunakula pamoja na kunywa kemikali za hatari na kuingiza katika miili yetu. Miili yetu hua inafanana sana na injini mfano magari.

Gari ni lazima ulifanyie service kama vile kubadilisha oil n.k kila baada ya muda flani. Vivyo hivyo na miili yetu, ni lazima kujifunza kuisafisha na kuondoa taka mwili ambazo huingia kupitia njia mbali mbali kila siku.

Katika mlo wako wa kila siku, kuna vyakula unaweza kuviongeza na vikasaidia sana kusafisha mwili wako kuanzia ndani.

1. Giligilani

Majani ya giligilani


Zina wingi wa vitakasa sumu (antioxidants) pamoja na Vitamin A, K pamoja na C, husaidia moyo, Figo pamoja na Ini kuondoa taka mwili ambazo hujishikiza humo.

Mafuta yaliyomo kwenye giligilani (volatile Oil) husawazisha seli zinazosababisha saratani.

Juisi ya giligilani husaidia sana afya ya macho pamoja na kuzuia uono hafifu wa macho kwa kuongeza mtiririko wa damu kwenye mishipa midogo midogo kwenye macho.

Tumia giligilani kama kiungo, juisi au chai mara kwa mara, na kisha uone matokeo utakayoyapata.

2. Kahawa

Kahawa


Kikombe kimoja cha kahawa asubuhi kinatosha kukusaidia kusafisha damu kwa siku, pia kinaweza kukupa nguvu za kukukinga dhidi ya magonjwa.

Kahawa ni moja kati ya dawa za kukuongezea nguvu kulingana na tafiti mbali mbali zilizofanywa na wataalam.

Kahawa inaweza kupunguza hatari ya kupatwa na magonjwa ya Ini pamoja na saratani, pia inauwezo wa kuzuia mafuta kuzidi mwilini na yasihifadhiwe na Ini, lakini hii ni kama utatumia kahawa bila kuweka sukari.

Unaweza kuweka mdalasini, mnanaa (mint), cocoa au tangawizi.

NB: usitumie kahawa kama una changamoto ya shinikizo la juu la damu (high blood pressure)

3. Green Tea

green tea


Matumizi ya mara kwa mara ya green tea husaidia kuongeza uchomwaji wa kalori mwilini pamoja na kupunguza mlundikano wa mafuta yanayozunguka Ini, Hivyo kusaidia kupunguza hatari ya saratani.

Unaweza kuongezea ndimu/limao au asali kwa ajili ya ladha. 

4. Manjano

manjano


Matumizi ya mara kwa mara husaidia kuondokana na shida nyingi za ki afya kutokana na uwepo wa curcumin ambayo ni anti-inflammatory.

Kupakaa kwenye kidonda husaidia kutokushambuliwa na bakteria na hivyo kusaidia kidonda kupona haraka,

Matumizi ya chai ya manjano au kuitumia kama kiungo husaidia sana afya ya ngozi na kufanya ngozi isiwe na chunusi, mzio, vipele pamoja na muwasho. 

5. Kabeji

kabeji


Linauwezo mkubwa wa kusawazisha free radicles katika mwili kutokana na wingi wa Magnesium, phosphorus, Vitamin C, Calcium pamoja na anti-oxidants.

Pia linapunguza hatari ya kupata saratani ya figo, lakini endapo haitapikwa kwa kuiva sana. Hivyo ni nzuri ikitumika kama kachumbari.

6. Beetroot

beetroot


zina wingi wa anti-oxidants na vitamins. Pia wingi wa Betalains na Nitrates ambazo hupunguza inflammation na oxidation.

7. Mboga za majani za kijani.

mboga za majani


Ni chakula bora zaidi duniani chenye wingi wa Vitamins muhimu ambazo husaidia mwili kufanya kazi kama mashine ambayo ina vilainishi bora.

Enzymes zake husaidia detoxification ya Ini, zina phytonutrients ambazo husaidia afya ya ngozi, kumbukumbu nzuri pamoja na tumbo lenye afya.

8. Tangawizi

Tangawizi


Huongeza ufanisi wa mzunguko wa damu hivyo damu kupata virutubisho vya kutosha kutoka kwenye chakula unachokula. Hii ni kutokana na uwepo wa Gingerol kwenye tangawizi.

Tangawizi husaidia kuondoa magonjwa ya Ini pamoja na kuongeza ufanisi wa kazi ya Ini na hivyo kuboresha usafishwaji wa damu unaofanywa na Ini.

Imeandaliwa na SAMUEL MACHA
FIT BY WAYNE

Simu: 0676068572/0753068572
whatsapp: 0621068072 au Bonyeza WHATSAPP

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed