Skip to main content

MADHARA 6 MAKUBWA YATOKANAYO NA KUNYWA SODA.

 

MADHARA 6 MAKUBWA YATOKANAYO NA KUNYWA SODA.

Soda hua ni kinywaji chenye sukari nyingi sana na kisicho na faida yoyote mwilini. (No nutritional value) ingawa watu wengi hupendelea kutumia katika nyakati tofauti.

Soda ni kinywaji chenye madhara mengi sana mwilini kuliko faida, na ni kinywaji ambacho ni vyema kukiepuka, ingawa watu wengi hupendelea hata kuwapa watoto watumie bila kujua ya kwamba wanahatarisha maisha yao ya sasa na baadae.

MADHARA YATOKANAYO NA KUNYWA SODA.

  • Ugonjwa wa Kimetabiliki (metabilic Syndrome): Matumizi ya Soda moja kwa siku huongeza hatari ya kupata ugonjwa wa kisukari kwa asilimia 67%
  • Afya ya Ngozi kudhoofika: Soda hua na kemikali inayoitwa Flame-Retardant Brominated Vegetable Oil (BVO), ni kemikali inayodhoofisha afya ya ngozi pamoja na mfumo wa neva za fahamu. 
  • Huongeza Kasi ya Uzee: Soda ina Phosphate pamoja na Phosphoric acid ambazo hutumika kufanya soda zikae muda mrefu bila kuharibika. Ila husababisha kuongezeka kwa kasi ya uzee na kusinyaa kwa ngozi.
  • Husababisha mishipa ya damu kukakamaa na kua migumu: kutokana na kuongezeka kwa mafuta ya Triglycerides kwa asilimia 30% pale unapokunywa soda moja kwa siku.
  • Huharibu Ubongo: soda ina mchanganyiko wa rangi za chakula (food dye), sukari nyingi ambayo ni aspartame. Hizi hua ni sumu katika seli za ubongo.
  • Unyeti wa meno (Tooth sensitivity) na Kuharibika kwa meno: soda zina Phosphoric acid pamoja na citric acid ambazo hubadilisha uwiano wa pH katika mdomo na kupelekea kuharibika kwa enamel ambayo inalinda jino.

Ni vyema kufanya maamuzi sahihi, hata kama wewe hujali afya yako, basi jitahidi usiwazoeshe watoto wako kunywa soda. Maji yanabaki kua kinywaji bora zaidi kuliko vyote.

Unapoenda ugenini, ukikaribishwa soda, hamna dhambi yoyote ukaomba maji. Sio lazima unywe soda unapokaribishwa, unaweza kuomba maji na ukafurahia afya yako.

Imeandikwa na SAMUEL MACHA
Mwanzilishi wa FIT BY WAYNE
Simu: 0753068572/0676068572
Whatsapp: 0621068072 

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...