Skip to main content

NAMNA YA KUFANYA MAZOEZI

 

Mazoezi

NAMNA YA KUFANYA MAZOEZI KWA AFYA.

Mazoezi ni shughuli yoyote ya mwili ambayo huongeza au kudumisha utimamu wa mwili, afya na ustawi kwa ujumla.

NI KWA NINI WATU HUFANYA MAZOEZI?

  • kusaidia ukuaji wa mwili
  • kuboresha nguvu ya mwili
  • kupunguza kasi ya uzee
  • kuboresha au kukuza misuli
  • kuboresha mfumo wa moyo na mishipa
  • kuboresha ujuzi wa riadha
  • kupunguza uzito/unene au kudumisha uzito sahihi
  • kuboresha afya
  • starehe na sababu nyinginezo

ISTILAHI MUHIMU ZA KUZIJUA

Kabla ya kuona jinsi ya kufanya mazoezi kadhaa, ni vyema kufahamu istilahi chache muhimu ambazo zitakuongoza katika ufanyaji mazoezi yako. Istilahi nyingine utaendelea kujifunza kadiri ynavyoendelea kubobea katika mazoezi.

REP: Hiki ni kifupisho cha neno Repeatition. katika mazoezi neno hili humaanisha kurudia kitendo flani. kwa mfano: mtu akisema 10 Reps, anamaanisha kufanya hicho kitendo husika mara 10. Kwa mtu ambae anapiga push up, akienda juu na chini amemaliza mara moja. hivyo 10 reps maana yake ni push ups 10.

SET: Hii ni kukamilisha marudio kadhaa ya zoezi husika kwa mpigo. kwa mfano mtu akipiga push up 10 kwa mpigo hapo tutasema amefanya set 1 ya zoezi la push up. hivyo akipiga push up 10 mfululizo, kisha akapumzika na kisha akapiga tena nyingine 10. Tutasema amepiga Set 2 za push up. lakini hapa tutaandika 2x10 (Set 2 zenye reps 10)

REST: Ni muda unaopumzika kati ya Set moja na Nyingine. Mara nyingi rest tunaziweka kwa sekunde, mfano mtu anaweza kuamua kupumzika sekunde 30 anapomaliza Set 1 kabla ya kwenda nyingine. Kwa mfano ukiona zoezi limeandikwa PUSH UP 2x10, 30 sec Rest. maana yake ni kwamba utapiga Set 2 za push up kila Set iwe na Reps 10, utapumzika kwa sekunde 30 baada ya kila set.

JINSI YA KUJUA KIWANGO CHA REPS KATIKA SET MOJA

Ikiwa unataka kufanya mazoezi, miili inatofautiana, kuna ambao wapo fit zaidi ya wengine katika ufanyaji mazoezi kulingana na sababu mbali mbali, hivyo kila mtu ni lazima ajue kiwango chake cha kuanzia. 

Jambo la kufanya, katika zoezi husika, fanya REPS nyingi kadiri unavyoweza mpaka mwili wako utakapokua hauwezi kuendelea tena. kisha zile REPS utagawanya kwa 3, na namba utakayoipata basi ndio REPS unazotakiwa kupiga katika kila SET.  Tazama mfano huu;

Tuseme unataka kujua kiwango cha Push up katika set husika. utakachofanya ni utapiga push up mpaka kufikia kikomo. tuseme utakua umepiga push up 30 ambapo utakua huwezi kuendelea tena kwa mara moja. 

Ukigawanya 30 kwa 3 utapata 10, maana yake katika kila SET yako inatakiwa iwe na REPS 10 za push up. Hivyo unaweza kufanya 3x10, 30 sec Rest (ikiwa na maana ya kwamba utapiga SET 3 ambazo kila SET itakua na REPS 10 za push up, utapumzika kwa sekunde 30 baada ya kila set.

BAADHI YA MAZOEZI MAZURI UNAYOWEZA KUYAFANYA.

Mazoezi ya kupunguza tumbo


Mazoezi ya kupunguza Unene

Mazoezi ya kupunguza unene

Mazoezi ya kupunguza nyama za mgongoni


Mazoezi ya kupunguza unene

Mazoezi ya kupunguza tumbo



Mazoezi ya kupunguza nyama za mikono

Jitahidi uwe unafanya mazoezi ambayo utayafurahia na unayaweza, usifanye mazoezi ambayo yatakuumiza sana.

Kumbuka kuanza taratibu, utakua unaongeza ukali wa mazoezi kadiri muda unavyokwenda. Nitakua naweka mazoezi kuongezea kila nitakapokua napata.

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed