Skip to main content

KWA NINI WATU WENYE UZITO MKUBWA HUHITAJI CHAKULA KINGI ZAIDI?

 

WATU WENYE UZITO MKUBWA HUHITAJI CHAKULA KINGI ZAIDI.

Bila shaka umeshawahi kusikia ama kuona neno CALORIE. Ikiwa na maana ya kiasi cha nishati kinachohitajika kuweza kuishi. 

Hapo awali tulielezea ya kwamba, endapo mtu utaingiza calorie nyingi kuliko unazotumia, basi utaongezeka uzito. Na pia kama utatumia calorie nyingi zaidi ya unazoingiza mwili basi utapungua uzito.

Kujua zaidi kuhusiana na Calorie kwenye vyakula tafadhali bonyeza HAPA (CALORIE ZA VYAKULA)

Tuangalie jambo moja, nalo ni BMR. Kirefu chake ni Basal Metabolic Rate.  Maana yake ni kiasi cha nishati kinachohitajika mwili kua hai wakati haufanyi shuhuli yoyote ile. BMR huchukua takribani 70% ya kiasi cha nishati kinachotumika kwa siku.

Sasa kila mwili wa mwanadamu una BMR yake kulingana na Uzito wake ulivyo. Wenye uzito mkubwa hua na BMR kubwa zaidi kulinganisha na wenye uzito mdogo. Lakini pia wanaume hua na BMR kubwa zaidi kulinganisha na wanawake.

Ili kuelewa zaidi kuhusiana na BMR, tazama mfano huu wa Bwanyenye...

Bwanyenye ni kijana mwenye uzito wa kilo 91. Kwa sasa BMR yake ni calorie 2500 akiwa ametulia bila kufanya chochote. Bwanyenye anachoshwa na uzito mkubwa, hivyo anafanya maamuzi ya kupunguza uzito kwa kubadilisha mtindo wake wa kula pamoja na kufanya maziezi.

Bwanyenye baada ya kufanikiwa kupunguza uzito, sasa ana kilo 73 na BMR yake ni calorie 2300 akiwa ametulia bila kufanya chochote.

Hivyo maana yake ni kwamba, Unapokua na uzito mkubwa zaidi, ndivyo jinsi unavyohitaji calorie nyingi ili uweze kuishi, na unapokua na uzito mdogo, unahitaji calorie chache zaidi.

Kadiri unavyopungua uzito au kuongezeka, na BMR yako hubadilika kutokana na kitu kinachoitwa Metabolic Adaptation. (hubadilika kulingana na uzito unaokua nao)

Ndio sababu kwa nini watu wanene au wenye uzito mkubwa mara nyingi hula sana kulinganisha na watu wenye uzito mdogo au wembamba.

Kwa msaada zaidi Juu ya kupunguza Unene

Whatsapp: 0621068072 au Bonyeza WHATSAPP

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed