Skip to main content

KWA NINI WATU WENYE UZITO MKUBWA HUHITAJI CHAKULA KINGI ZAIDI?

 

WATU WENYE UZITO MKUBWA HUHITAJI CHAKULA KINGI ZAIDI.

Bila shaka umeshawahi kusikia ama kuona neno CALORIE. Ikiwa na maana ya kiasi cha nishati kinachohitajika kuweza kuishi. 

Hapo awali tulielezea ya kwamba, endapo mtu utaingiza calorie nyingi kuliko unazotumia, basi utaongezeka uzito. Na pia kama utatumia calorie nyingi zaidi ya unazoingiza mwili basi utapungua uzito.

Kujua zaidi kuhusiana na Calorie kwenye vyakula tafadhali bonyeza HAPA (CALORIE ZA VYAKULA)

Tuangalie jambo moja, nalo ni BMR. Kirefu chake ni Basal Metabolic Rate.  Maana yake ni kiasi cha nishati kinachohitajika mwili kua hai wakati haufanyi shuhuli yoyote ile. BMR huchukua takribani 70% ya kiasi cha nishati kinachotumika kwa siku.

Sasa kila mwili wa mwanadamu una BMR yake kulingana na Uzito wake ulivyo. Wenye uzito mkubwa hua na BMR kubwa zaidi kulinganisha na wenye uzito mdogo. Lakini pia wanaume hua na BMR kubwa zaidi kulinganisha na wanawake.

Ili kuelewa zaidi kuhusiana na BMR, tazama mfano huu wa Bwanyenye...

Bwanyenye ni kijana mwenye uzito wa kilo 91. Kwa sasa BMR yake ni calorie 2500 akiwa ametulia bila kufanya chochote. Bwanyenye anachoshwa na uzito mkubwa, hivyo anafanya maamuzi ya kupunguza uzito kwa kubadilisha mtindo wake wa kula pamoja na kufanya maziezi.

Bwanyenye baada ya kufanikiwa kupunguza uzito, sasa ana kilo 73 na BMR yake ni calorie 2300 akiwa ametulia bila kufanya chochote.

Hivyo maana yake ni kwamba, Unapokua na uzito mkubwa zaidi, ndivyo jinsi unavyohitaji calorie nyingi ili uweze kuishi, na unapokua na uzito mdogo, unahitaji calorie chache zaidi.

Kadiri unavyopungua uzito au kuongezeka, na BMR yako hubadilika kutokana na kitu kinachoitwa Metabolic Adaptation. (hubadilika kulingana na uzito unaokua nao)

Ndio sababu kwa nini watu wanene au wenye uzito mkubwa mara nyingi hula sana kulinganisha na watu wenye uzito mdogo au wembamba.

Kwa msaada zaidi Juu ya kupunguza Unene

Whatsapp: 0621068072 au Bonyeza WHATSAPP

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...