Skip to main content

NJIA RAHISI JINSI YA KUANZA KUPUNGUZA UNENE/KITAMBI

 

NJIA RAHISI JINSI YA KUANZA KUPUNGUZA UNENE/KITAMBI.

Inakadiriwa ya kwamba, katika kila familia hapa Tanzania, hapakosekani walau mtu mmoja ambae ana uziro uliopitiliza. Yaani Obese.

Wapo watu kadhaa ambao wamekua wakisema ya kwamba wao wana unene wa kurithi. Kwa sababu katika familia au ukoo wao wengi ni wanene. Lakini hili halina ukweli, Ila tu ni kwamba familia nyingi zinarithishana mtindo wa maisha. Na hivyo ndio maana unaweza kuona familia flani au ukoo flani wote ni wanene.

Inapokuja swala la kupunguza unene, hamna njia za mkato kama ambavyo watu wengi hupendelea. Mtu anasahau ya kwamba hakunenepa ndani ya muda mfupi, bali alinenepa kwa muda mrefu. Lakini leo hii mtu atataka kupungua haraka sana ndani ya muda mfupi. ROMA HAIKUJENGWA KWA SIKU MOJA.

Njia bora zaidi ya kupunguza Unene ni kwa kuzingatia ulaji sahihi pamoja na kubadilisha mtindo wa maisha kwa ujumla.

Zipo dawa zinazosaidia kurahisisha safari ya kupunguza unene, lakini ieleweke ya kwamba, dawa hizi husaidia kurahisisha. lakini usipobadilisha mtindo wa kula na wa maisha, utakua huna tofauti na mtu ambaye amefua nguo nyeupe na kisha kuitupa kwenye matope.

JINSI YA KUANZA KUPUNGUZA UNENE/KITAMBI

  • Anza kwa kupunguza wingi wa chakula cha wanga. (haswa wanga uliokobolewa). Kama ulikua umezoea kupakua chakula cha kiwango flani, anza kupunguza nusu sahani.
  • Anza kuweka mboga nyingi za majani na matunda. (Hapa wanga uwe kiasi kama cha ngumi ya mkono wako)
  • Punguza matumizi ya sukari. kama ulikua ukitumia vijiko viwili au zaidi, anza kwa kuweka kijiko kimoja pekee. (kumbuka sukari husababisha unene zaidi kuliko hata mafuta)
  • Kunywa maji glasi moja walau nusu saa (dakika 30) kabla ya kula chakula. Hii itakusaidia kupata shibe mapema.
  • Tumia sahani ndogo kupakua chakula chako. kwani Sahani kubwa itaudanganya ubongo wako ya kwamba chakula ni kidogo wakati ni kingi.
Endapo ukizingatia maagizo hayo, taratibu utaanza kuona mwili wako unabadilika wiki hadi wiki. kikubwa ni ujifunze kua na subira kwani ROMA HAIKUJENGWA KWA SIKU MOJA.

Kama utapendelea kupata Programu nzuri ya kuweza kupunguza Unene. Wasiliana nami kwa namba 0753068572 au Whatsapp 0621068072. au Bonyeza HAPA

Imeandikwa na SAMUEL MACHA, FIT BY WAYNE.

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...