Skip to main content

VYAKULA VINAVYOSAIDIA KUTIBU TATIZO LA GAUTI

 

Gauti (Gout)

GAUTI NI NINI?

Gauti ni aina ya ugonjwa unaoathiri viungo vya mwili na husababishwa na kuwepo kwa kiasi kikubwa cha tindikali ya urea (excessive Uric Acid) katika damu.

Tindikali ya urea (uric acid) hutokea kama taka mwili inayokuwepo kwenye damu. Tindikali hii hutengenezwa pale ambapo mwili huvunja kemikali ya Purin wakati wa umeng"enyaji wa chakula na hivyo kubaki kwenye damu.

SABABU ZA HATARI KUPATA GAUTI.

  • Wanaume hupata Gauti zaidi kuliko wanawake.
  • Uzito mkubwa/ unene huongeza hatari ya kupata gauti
  • Baadhi ya magonjwa kama vile magonjwa ya moyo, magonjwa ya figo pamoja na kisukari.
  • Baadhi ya dawa
  • Matumizi ya pombe.
  • Vyakula vyenye kiwango kikubwa cha Purine kama vile Nyama nyekundu.

DALILI ZA GAUTI

  • Maumivu makali kwenye viungo, haswa kidole kikubwa cha mguu, goti au mguu (ankle)
  • Kuvimba vya sehemu ya kiungo
  • Sehemu yenye shida kua nyekundu na ya moto.

VYAKULA VINAVYOSAIDIA KUTIBU NA KUZUIA TATIZO LA GAUTI.

NB: kabla ya kuangalia vyakula hivyo, njia rahisi na ya haraka zaidi ni Kupunguza uzito uliozidi, kuacha matummizi ya vitu vya sukari pamoja na kuacha matumizi ya pombe.

  • Matunda na mboga za majani: zina kiwango kidogo cha purin na wingi wa Vitamin C.
  • Tufaa (Apple): hua na compound maalum iitwayo Malic Acid inayosawazisha kiwango cha tindikali ya Uric kwenye damu.
  • Mafuta ya Zeituni (Olive Oil): ina anti oxidants nyingi pamoja na anti inflammation.
  • Vyakula vyenye nyuzinyuzi: mfano Oats, Maharage, Parachichi na njegere. Husaidia kuchochea bakteria wazuri wa kwenye tumbo kupunguza inflammation.
  • Limao/Ndimu: hua na vitamin C ambayo huyeyusha Uric acid.
  • Apple Cider Vinegar (siki ya tufaa): huyeyusha chembe chembe za uric acid kwenye damu endapo utatumia mara 2 au 3 kwa siku, (unatumia kwa kuchanganya kijiko kimoja na kikombe cha maji)
  • Maji: husaidia kuyeyusha uric acid iliyozidi.
  • Vyakula Vya Vitamin C: mfano machungwa, nanasi na papai. Hupunguza inflammation.
  • Tango: ina tabia ya detox inayosaidia kuyeyusha uric acid.
Ipo tiba iliyoandaliwa kwa ajili ya Uric Acid. kwa msaada zaidi juu ya Tiba hiyo tafadhali bonyeza HAPA kisha tuma Ujumbe wa URIC ACID.

Mawasiliano:

  • 0753068572 (simu)
  • 0621068072 (whatsapp)

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   ๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1๏ธโƒฃHistoria ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2๏ธโƒฃKupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3๏ธโƒฃUnene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4๏ธโƒฃKu...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (ยฐC). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...