Skip to main content

VIRUTUBISHO 6 VYENYE AFYA

 

VIRUTUBISHO 6 VYENYE AFYA

Virutubisho ni dutu (substance) ambazo hurutubisha mwili na afya kwa ujumla. Virutubisho hupatikana kwenye vyakula tunavyokula au kunywa kila siku. 

Japokua, kila tunachokula au kunywa, hytofautiana virutubisho vinavyopatikana. Kuna ambavyo vimejaa virutubisho, na kuna ambavyo havina virutubisho na hivyo kua havina faida kwenye mwili wa mwanadamu ingawa vinaonekana kua na ladha nzuri.

VIRUTUBISHO 6 VYENYE AFYA NA VYAKULA VYAKE.

1. NYUZI NYUZI

Nyuzi nyuzi husaidia sana kuratibu uzito wa mwili, kupunguza hatari za kisukari na lehemu (cholesterol) kwenye damu, Pia kupunguza athari za magonjwa ya moyo.

Nyuzi zisizo yeyuka husaidia sana kuweka mfumo wa chakula na msukumo uende kwa urahisi.

vyakula Vyenye nyuzi nyuzi ni kama vile Njegere, karoti, maharage mabichi, cauliflower, viazi vitamu, matunda

2. VITAMIN A

Husaidia sana kuona kwa macho na kukinga mwili dhidi ya magonjwa ya kuambukiza. Pia husaidia kuwezesha nyama za mifupa, ngozi na meno kuwa na afya nzuri.

Vyakula vyenye Vitamin A ni kama vile; Matunda yenye rangi ya pink, brokoli, spinachi, aprikoti, viazi vitamu, mboga za majani, mayai n.k

3. VITAMIN C

Husaidia sana kuimarisha mfumo wa mifupa kama meno, mifupa, mifupa laini (cartilage). Husaidia kuponya vidonda na kujenga protini na mishipa ya damu na ngozi katika kidonda.

Husaidia pia kunyinywa kwa madini ya chuma, hulinda miili yetu dhidi ya chembechembe zinazotokana na kuunguzwa kwa chakula mwilini (free radicals)

Vyakula vyenye Vitamin C ni kama vile; Cauliflower, kabichi, viazi vitamu, brokoli, maembe, matikiti maji, mananasi, mapapai, machungwa, zabibu na hoho nyekundu.

4. MADINI YA CHUMA

Husaidia mishipa ya damu kuhifadhi hewa ya oksijeni na kuitumia. Madini ya chuma hupatikana kwenye chembechembe nyekundu za damu ambayo husafirisha oksijeni mwilini.

Vyakula ni vyenye madini ya chuma ni kama vile; Maboga, spinachi, maharage, mboga za majani, nyama nyekundu, maini (ila epuka wakati wa ujauzito), n.k

5. ANTIOXIDANTI (ANTI OXIDANTS)

Hulinda mwili dhidi ya chembechembe (free radicals) zinazotolewa wakati wa kusagwa chakula mwilini ambapo huungana nazo na kuondoa uharibifu wake.

Free radicals husababisha kupungua kwa nguvu za kioo cha macho, maumivu ya viungo (arthritis), uharibufu wa mishipa ya ubongo (nerves) inayoleta ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu (Alzheimer), zinaongeza hatari ya magonjwa ya moyo, zinaharakisha uzee na kusababisha magonjwa ya saratani kwa kuharibu seli za DNA.

NB: DNA (Deoxyribo Nucleic Acid) hutoa maelekezo ya urithi wa Tabia au umbile katika kizazi.

6. OMEGA-3

Zipo zinazotokana na mimea na inayotokana na samaki au mayai.
Omega-3 za mimea hupatikana kwenye mbegu za chia, mbegu za maboga, walnuts, maharage meupe yaliokaushwa, maharage ya soya machanga yaliyopikwa na maganda yake.

Omega-3 zinazotokana na samaki hupatikana kwenye dagaa, jodari, sangara na vibua. Pia mayai yana kiwango kidogo cha Omega-3

Mpaka kufikia hapo, utakua umeelewa kitu kuhusu virutubisho ambavyo vinafaida kubwa mwilini. Na utakua umejua ni vyakula gani utumie ili kufaidika kwa kupata virutubisho hivyo.

By Samuel Macha (FIT BY WAYNE)

Mobile: 0753068572
whatsapp: 0621068072 au Bonyeza WHATSAPP

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed