Skip to main content

SABABU 15 KWA NINI UNAONGEZEKA UZITO.

 

kwa nini unaongezeka uzito.

SABABU 15 KWA NINI UNAONGEZEKA UZITO

yawezekana umekua ukifanya mazoezi na kutafuta njia kadhaa za kuweza kupunguza uzito ambao umezidi, ila mara nyingi unakwama na hufikii malengo yako.

Huenda ni kwa sababu hujazijua sababu hizi zinazosababisha kuongezeka kwa uzito.

1. KUTOKUPATA USINGIZI WA KUTOSHA

Haswa wakati wa usiku, hii husababisha kitu kinaitwa LOWER RESTING METABOLIC RATE

2. MVURUGIKO WA HOMONI (HORMONAL IMBALANCE)

Homoni au vivhochezi ndio husaidia kukontrol mwili na yanayotokea mwilini, hivyo zinapokua hazipo katika uwiano unaotakiwa, hupelekea mwili kuongezeka uzito kwa baadhi ya watu.

3. WATER RETENTION (MAJI YANAYOBAKI MWILINI BILA KUTOKA)

Mwili wako unapohifadhi maji mwilini bila kutumika, utagundua ya kwamba uzito unaongezeka. Hii ni kwa sababu maji pia yana uzito, hivyo yanavyozidi kua mengi mwilini, na uzito unaongezeka. Moja ya sababu zinazopelekea hali hii ni utumiaji wa chumvi nyingi, pia baadhi ya dawa, kubadilika kwa homoni, au baadhi ya hali za ki afya.

4. STRESS/DEPRESSION (MSONGO WA MAWAZO/SONONA)

Unapokua katika hali hii, mwili wako hua unaachilia homoni ya cortisol unapokua na stress kwa muda mrefu pamoja na adrenaline. unapokua na mashaka au wasiwasi, hizi homoni hujiandaa kuweka mwili wako katika hali ya SURVIVAL MODE, inayopelekea mwili kutunza mafuta.

5. KULA ZAIDI YA KIWANGO CHA KAWAIDA

Hata kama chakula ni chenye afya, unatakiwa ule kiasi cha kawaida kitakachokufanya ushibe na sio kuvimbiwa. Yawezekana vyakula unavyokula vina calorie chache, ila ukumbuke ya kwamba CHEMBE NA CHEMBE MKATE HUWA.

6. KUTANUKA AU KWA MISULI

Kuna baadhi ya mazoezi hufanya misuli itanuke zaidi, na kutanuka kwa misuli maana yake hata uzito unaongezeka.

7. MARA BAADA YA KUACHA SIGARA

Mara nyingi mtu anapoamua kuachana na sigara, anaweza kuona anaongezeka mwili au uzito kidogo, Hivyo ni vyema mtu huyu akatumia mboga mboga kwa wingi pamoja na maji.

8. KUCHELEWA KULA MLO WA JIONI.

Unapokula chakula chini ya masaa matatu kabla ya kwenda kulala, mwili hautapata muda wa kuyeyusha chakula tumboni pamoja na zile calorie ambazo umeingiza.

9. USAFI MBOVU WA KINYWA.

Mwili wa mwanadamu umeunganika katika maeneo mengi, inapotokea ukapata kichochezi (inflammation) kwenye fizi, basi na sehemu nyingine za mwili zinakua kama zimepata hiyo shida na kuanza kuhifadhi mafuta.

10. KUTUMIA ZAIDI VYAKULA VYA KUNUNUA KULIKO KUANDAA NYUMBANI

Mara nyingi vyakula vya kununua kwa asilimia kubwa sio rafiki na huongeza uzito, hivyo unapokula kila siku, HABA NA HABA HUJAZA KIBABA.

11. KULA CHAKULA KINGI BAADA YA MAZOEZI

Unaweza usijue ni kiasi gani cha calorie umetumia wakati wa mazoezi, na pia usijue kiwango cha calorie utakachoingiza punde tu utakapokula chakula hicho

12. UKOSEFU WA MAJI MWILINI (DEHYDRATION)

Itapunguza ufanisi wa kimetaboliki na jinsi mwili wako unavyochoma mafuta. Hii itakufanya calorie unazoingiza ziwe nyingi kuliko unazozitoa.

13. UTUMIAJI WA JUISI NA VINYWAJI (ISIPOKUA MAJI)

Watu wengi hua hwahesabu kitu kinachoitwa LIQUID CALORIE, kama vile juisi, bia, mvinyo, kahawa n.k.

Hali hii hupelekea kuingiza calorie nyingi zaidi kwa siku kuliko mwili unavyotumia, kwa sababau ni rahisi zaidi kunywa kuliko kunywa.

14. UCHAFUZI WA  HEWA

Tafiti zinaonyesha ya kwamba watu wanaoishi maeneno ambayo kuna uchafuzi mkubwa wa hewa hujikuta na uzito mkubwa zaidi na hatari ya magonjwa ya moyo kuliko wale ambao wanaishi sehemu ambazo hazina uchafuzi huo.

Ndio maana katika program nilizotoa hapo awali, tulianza na Detox kwanza kwa ajili ya kutoa taka mwili kutoka kwenye miili yetu.

15. KUISHI BILA KUJUA UZITO WAKO MARA KWA MARA

Wewe una kilo ngapi??? Watu wengi ukiwauliza swali hili, watakujibu hivi... MARA YA MWISHO ILIKUA..... maana yake hana uhakika sasa hivi anazo ngapi. Kujua uzito wako mara kwa mara itakusaidia kujua wapi upunguze na wapi uache. kwa sababu uzito ukiongezeka taratibu hutajua, ni siku tu itatokea mtu anakwambia... FLANI UMENENEPA... na wewe unaanza kushangaa.

Imeandikwa na SAMUEL MACHA
FIT BY WAYNE

CONTACTS
Mobile: 0753068572

kwa msaada zaidi juu ya kupunguza uzito
whatsapp: 0621068072, au Bonyeza WHATSAPP

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed