Skip to main content

USITUMIE VYAKULA HIVI KAMA UNA UMRI WA MIAKA 30 AU ZAIDI

 

USILE VYAKULA HIVI KAMA UNA UMRI WA MIAKA 30 AU ZAIDI 

'The doctors of the future will no longer treat the human frame with drugs, but rather will cure and prevent disease with nutrition’ - Thomas Edison. 

Lishe ndio kitu kikubwa Zaidi katika kuboresha au kubomoa afya ya mwanadamu. Na kwa kutumia lishe pekee, una uwezo wa kufanya mwili wako uwe na uwezo mkubwa wa kujitibu wenyewe.

Kama una umri (au utakapofikisha umri) wa miaka 30 na Zaidi, basi vyakula hivi jitahidi kuviepuka. 

  •  Pombe : hua ina kalori nyingi sana, na kuanzia umri wa miaka 30 mwili hauwezi tena kuzichoma zote na hivyo kuhifadhiwa kama mafuta na kusababisha kitambi/unene. Pia inabadilisha kiwango cha insulini na kusababisha kua na hamu ya kula vitu vyenye sukari.

  •  Sukari za kutengenezwa: hizi husababisha mwili wako usitumie kalori zake vizuri na pia huongeza hatari ya saratani. Pia husababisha glucose kuwepo kwa kiwango kikubwa na kupunguza ufanisi wa insulini. Hivyo kusababisha kuongezeka kwa uzito, magonjwa ya moyo na kisukari.

  • Caffeine : hii husababisha kuzeeka mapema na pia kusababisha kua na hamu ya kula vitu vya sukari inayopelekea kuongezeka kwa uzito/kitambi.

  • Ngano iliyokobolewa : mwili wako unageuza ngano hii kua glucose na hivyo kuhifadhiwa mwilini kama mafuta. Hivyo ni vyema kutumia ngano ambayo haijakobolewa.

  • Mtindi ulioongozewa ladha bandia : bila shaka unafahamu yogurt za viwandani zenye ladha ya strawberry, chocolate, vanilla n.k hizi hua na sukari nyingi sana ambayo sio nzuri kwako

  • Maziwa : vyakula vitokanavyo na wanyama hua na kiwango kikubwa cha acid. Na maziwa mengi hua yanasafishwa ili kuua vijidudu ambapo hupelekea kuua na virutubisho. (kwa maziwa ya viwandani)

  • Vyakula vya kwenye makopo : hivi hua na kiwango kikubwa cha sukari, chumvi na mafuta. Na vyote hivi sio vizuri kwa afya.

  • Soda : ina kiwango kikubwa cha sukari ya fructose corn syrup ambayo ni mbaya sana kwa afya kwa sababu yenyewe huenda moja kwa moja kwenye ini na kuhifadhiwa kama mafuta (fat). Pia husababisha mwili usitumie leptin (leptin resistance) ambayo ni hormone inayofanya uwiano wa hamu ya kula na kufanya uwe na kiu ya soda Zaidi au vitu vya sukari. Na hii ndio hupelekea kunenepa Zaidi na kua na kitambi.


 THE BEST KEPT SECRET OF MEDICINE IS THAT, THE BODY HEALS ITSELF IF WE CREATE THE RIGHT CONDITIONS.

Imeandikwa na SAMUEL MACHA, 

FIT BY WAYNE.

CONTACTS: Mobile 0753068572, whatsapp WHATSAPP

Comments

  1. Mungu akuzidishie umri unasaidia wengi

    ReplyDelete
    Replies
    1. Huwa natumia maziwa fresh na mhogo wa kuchemshwakutwa nikisickia njaa huwa nakula parachichi je ninakosea naomba msaada wako

      Delete
  2. Mungu akuongezee maarifa tuzidi kupata elimu

    ReplyDelete
  3. Hapo Kwenye maziwa,ugonjwa 🤔🤔🤔

    ReplyDelete
  4. Asante kwa darsa mungu akulipe hitaj lako

    ReplyDelete
  5. ahsante Sana sijawahi kujutia kukujua

    ReplyDelete
  6. Asante Sana Dr.... Binafsi umenisaidia Sana

    ReplyDelete
  7. Mm soda nilisha acha hata chai nina muda mrefu sana sijanywa

    ReplyDelete
  8. Mungu akubariki Mdogo wangu Samwel,,,Sijutii kukufahamu!

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Ku...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (°C). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...