Skip to main content

MLO SAHIHI KULINGANA NA KUNDI LA DAMU (BLOOD GROUP)

 

MLO SAHIHI KULINGANA NA KUNDI LAKO LA DAMU (BLOOD GROUP)

Kuna msemo unaosema kua ONE MAN'S FOOD IS ANOTHER MAN'S POISON. Yaani ikiwa inamaanisha kua. Chakula ambacho kina manufaa kwako, huenda kikawa ni sumu kwa mtu mwingine.

Sasa najua utajiuliza kua kwa nini ipo hivi. Hii ni kwa sababu sisi tupo vile tulivyo kulingana na kundi la damu tulilo nalo. Damu ni uhai, damu haielezeki kiurahisi. Lakini ndio inatupa uhai sisi binadamu na viumbe vingine vyote. Lakini je, kutokana na makundi ya damu tuliyonayo, ni sahihi kila kundi kula mlo mmoja??

Labda nitoe mfano kidogo; Blood group O wanafanya vizuri sana wakila protini kama nyama, kwa sababu hawa hua wana acid nyingi tumboni, na ndio maana Blood Group O wengi wana vidonda vya tumbo.

Lakini blood group A wanafanya vizuri sana kama wakila mboga za majani. Kwa sababu wakila nyama inawatesa kwenye mmeng'enyo wa chakula na huhifadhiwa kama mafuta mwilini. Hii ni kwa sababu wana acid ndogo sana tumboni, ndio maana Blood Group A wengi wanasadikiwa kua na hatari kubwa ya kupata saratani.

Lakini endapo utakula kulingana na kundi lako la damu lilivyo. Utapata faida nyingi sana. Faida utakazopata kama ukila kulingana na kundi lako la damu ni kama ifuatavyo;

  • 1.      Utaondokana na maambukizi ya kawaida ya virusi au bacteria.
  • 2.    Utapungua uzito (utakua na uzito sahihi) kwa sababu mwili utaondoa sumu (toxins) na mafuta yaliyojilundika mwilini.
  • 3.      Utaweza kupambana na magonjwa yanayo hatarisha maisha kama vile magonjwa ya moyo, kisukari pamoja na magonjwa ya ini.
  • 4.      Utaepukana na visababishi vya kuharibu cell za mwili. Hivyo kasi yako ya kuzeeka itapungua sana.

Vyakula kulingana na kundi lako la damu vimegawanyika katika sehemu kuu tatu (3);

  • 1.      VYENYE MANUFAA SANA = hivi ni vyakula ambavyo ni dawa kwako
  • 2.      VYA UPANDE WOWOTE (NEUTRAL) = hivi ni vyakula ambavyo ni chakula tu, havina madhara wala faida kubwa.
  • 3.      VYA KUEPUKA = hivi ni vyakula ambavyo kwako ni sumu.

BLOOD GROUP O (THE HUNTER)

Hili ndio kundi kongwe Zaidi kutokea duniani. Inakadiriwa kua Group O walikuepo tangu miaka ya 50,000 BC. Hawa wanaitwa wala nyama au wawindaji. (the hunters).

Hawa wana mfumo wa chakula ambao ni mgumu kiasi na wanafanya vizuri sana kama wakila protini za juu kama vile nyama. Na hua wanatakiwa kufanya mazoezi makali, na hii hua inawasaidia kukabiliana na stress.

Group O wana kiwango kikubwa sana cha acid mwilini, na ndio maana wanahitaji protini nyingi. Lakini pia ndio sababu kwa nini wengi wao husumbuliwa na vidonda vya tumbo.

VIFUATAVYO NI VYAKULA AMBAVYO VINAFANYA BLOOD GROUP O WANENEPE;

  • 1.      Gluteni ya ngano; hii inaingiliana na uzalishwaji wa insulin mwilini na hivyo kufanya mfumo wa kimetaboliki (metabolism) kua hafifu.
  • 2.      Mahindi ya nafaka (sweetcorn); hii huingilia uzalishwaji wa insulin na hivyo kufanya kimetaboliki kua hafifu. (Ni mahindi ambayo huvunwa kabla ya kukomaa vizuri, na yanakua kama yana sukari au matamu).
  • 3.      Maharagwe ya figo (kidney bean), maharagwe ya navy na lenti (lori); haya hufanya utumiwaji wa kalori mwilini kua hafifu.
  • 4.      Kabeji, Brussel, koulifulawa (cauliflower), majani ya haradali; hizi huzuia uzalishwaji wa hormone ya thyroid.

 

VIFUATAVYO NI VYAKULA AMBAVYO HUSAIDIA BLOOD GROUP O WAWEZE KUPUNGUA UZITO;

  • ·         Kelp (aina ya algae inayoota pembezoni mwa bahari), vyakula vya baharini, chumvi yenye iodine; hivi vina iodine ambayo inaongeza uzalishwaji wa hormone ya thyroid mwilini.
  • ·         Maini; yana vitamin B ambayo yanasaidia ufanisi wa kimetaboliki.
  • ·         Nyama nyekundu, mboga ya kale, spinachi, broccoli; hizi husaidia ufanisi wa kimetaboliki.

JINSI YA KULA KWA BLOOD GROUP O.

  • ·         NYAMA ZENYE MANUFAA SANA; nyama ya ng‘ombe, moyo, figo, nyama ya kondoo, maini, utumbo (taulo), mkia, swala.
  • ·         NYAMA ZA KUEPUKA; nguruwe, goose (bata Bukini)
  • ·         VYAKULA VYA BAHARINI VYENYE MANUFAA; blue fish, cod fish (samaki chewa), sword fish.
  • ·         VYAKULA VYA BAHARINI VYA KUEPUKA; baraccuda, cat fish, pweza, smoked salmon (samaki saroni), cavier, conch (samaki kondomu).
  • ·         VYAKULA VITOKANAVYO NA MAZIWA; Group O wanatakiwa kujitahidi kutokutumia vyakula hivi. Ila wanaweza kutumia soya kama mbadala
  • ·         VYAKULA VITOKANAVYO NA MAZIWA VYA KUEPUKA; jibini (cheese), maziwa ya mbuzi, ice-cream, skimmed milk, mgando (frozen yogurt)
  • ·         Group O wanafanya vizuri kwenye oils na fats
  • ·         MAFUTA YENYE MANUFAA ZAIDI; mafuta ya zeituni (olive oil), flaxseed oil.
  • ·         MAFUTA YA KUEPUKA; mafuta ya nafaka (corn oil), mafuta ya mbegu za pamba, mafuta ya njugu, mafuta ya alizeti.
  • ·         MBEGU ZENYE MANUFAA ZAIDI; mbegu za maboga, walnuts (jozi)
  • ·         MBEGU ZA KUEPUKA; korosho, karanga, siagi ya karanga.
  • ·         MAHARAGE YENYE MANUFAA ZAIDI; aduki beans (yapo asia kwa sana), black eyed beans.
  • ·         MAHARAGWE YA KUEPUKA; maharagwe ya figo, maharagwe ya navy, lenti, maharagwe ya soya.
  • ·         MBOGA ZENYE MANUFAA; broccoli, kitunguu swaumu, kale, vitunguu maji, viazi vitamu, pasrley (mboga za pasile), pilipili, maboga spinachi.
  • ·         MBOGA ZA KUEPUKA; parachichi, kabichi, koulifulawa, uyoga, viazi, zeituni, sweetcorn.
  • ·         MATUNDA YA KUEPUKA; nazi, blackberries, tikiti, machungwa, strawberries, plantains (ndizi za kupika)
  • ·         VINYWAJI VYA KUEPUKA; kahawa, soda

BLOOD GROUP A (THE CULTIVATORS)

      Hawafanyi vizuri wakila protini za nyama. (zinaongeza mucus {belaghami} kwenye mfumo wao wa hewa) ila wanafanya vizuri sana kwenye protini za mimea kama soya na tofu

      Ndio wa kwanza kutumia mbogamboga

      Mfumo wao wa chakula upo sensitive sana

      Wanadili na stress kwa vitendo vya utulivu kama yoga.

      Wana hatari kubwa ya magonjwa ya moyo, saratani na kisukari ki biologia.

      Wanahifadhi nyama mwilini kama mafuta

      Wana acid ndogo sana tumboni

      Vyakula vitokanavyo na maziwa sio vizuri sana kwao

 

VYAKULA VINAVYOPELEKEA GROUP A KUONGEZEKA UZITO.

      Nyama; haimeng‘enywi vizuri na inahifadhiwa kama mafuta.

      Vyakula vya maziwa; vinachochea reaction ya insulin na hupelekea kimetaboliki kua hafifu.

      Maharagwe ya lima; yanafanya kimetaboliki kua hafifu.

      Ngano(ya kias kikubwa); inafanya misuli kua na acid, hivyo kufanya uhafifu wa matumizi ya kalori.

VYAKULA VINAVYOPELEKEA GROUP A KUPUNGUA UZITO.

      Mafuta ya mboga (vegetable oil); yanawezesha mmeng‘enyo mzuri, yanasaidia kuzuia maji mengi kubaki mwilini. (fluid retention)

      Vyakula vya soya; vinawezesha mmeng‘enyo mzuri wa chakula, kimetaboliki kua na ufanisi, vinaweka sawa kinga ya mwili.

      Mbogamboga; zinafanya ufanisi mzuri wa kimetaboliki.

      Nanasi; inaongeza ufanisi wa tumbo, inaongeza ufanisi wa utumiaji wa kalori.

      Group A wanafanya vizuri kama wasipotumia nyama, ila wanaweza kutumia samaki badala ya nyama.

ULAJI WA VYAKULA KWA GROUP A.

      NYAMA ZA KUEPUKA; nguruwe, kondoo, maini, nyama ya ng‘ombe, bata, moyo, figo.

      VYAKULA VYA BAHARINI; ni vizuri sana kwa Group A

      VYAKULA VYA BAHARINI VYA KUEPUKA; barracuda, bluefish, catfish, kaa, lobster (Kambamti), pweza, ngisi.

      VYAKULA VYA MAZIWA; hawapaswi kutumia chochote kilichotengenezwa na whole milk au mayai. Ila wanaweza kutumia maziwa ya soya na jibini ya soya kama mbadala.

      VYAKULA VYA MAZIWA VYA KUEPUKA; jibini, siagi, ice-cream, maziwa.

      OIL & FAT ZENYE MANUFAA; mafuta ya flaxseed (kitani), mafuta ya zeituni

      MAFUTA YA KUEPUKA; corn oil (mafuta ya nafaka), mafuta ya mbegu za pamba, mafuta wa njugu, mafuta ya sesame (ufuta)

      MBEGU ZENYE MANUFAA; karanga(nzuri kwa kupigana na seili za saratani), siagi ya karanga, mbegu za maboga.

      MBEGU ZA KUEPUKA; korosho.

      MAHARAGWE YENYE MANUFAA; maharagwe ya adzuki, maharagwe meusi, maharagwe mekundu ya soya

      MAHARAGWE YA KUEPUKA; kidney beans, maharagwe ya lima, maharagwe ya Navy, maharagwe mekundu.

      VYAKULA VYA NAFAKA VYENYE MANUFAA; buckwheat (ngano isiyo na gluten), amaranth, unga wa mchele, unga wa oat,

      NAFAKA ZA KUEPUKA; cream ya ngano, wheat bran, unga wa ngano (whole wheat flour)

      MBOGAMBOGA ZENYE MANUFAA; broccoli, kitunguu swaumu, kale, kitunguu maji, tofu, maboga, spinachi.

      MBOGAMBOGA ZA KUEPUKA; kabichi, pilipili ya chili, uyoga, zeituni, viazi, nyanya, magimbi.

      MATUNDA YENYE MANUFAA; grapefruit, limao/ndimu, nanasi

      MATUNDA YA KUEPUKA; ndizi mbivu, nazi, machungwa, ndizi za kupika, maembe, tikiti, papai.

      VINYWAJI VYENYE MANUFAA; mvinyo mwekundu (red wine) ni nzuri kwa afya ya moyo, kahawa, green tea.

      VINYWAJI VYA KUEPUKA; bia, spirit, chai, soda.

BLOOD GROUP B (THE NOMAD)

      wapo na balance (kama jina lao)

      Wana kinga yenye nguvu

      Wanauwezo wa kula vitu vingi tofauti Zaidi, walaji wa vyakula vitokanavyo na maziwa.

      Wanadili na stress kwa kufanya shughuli za ubunifu.

      Wanauwezo wa kushinda magonjwa mengi makubwa kama magonjwa ya moyo na saratani

      Ni rahisi kupata matatizo yanayotokana na udhaifu wa kinga ya mwili kama vile chronic fatique syndrome (ugonjwa wa kuchoka sana), multiple sclerosis (ugonjwa unaokula nerves), lupus (kinga ya mwili inakula tissue zake zenyewe)

VYAKULA VINAVYOWAONGEZEA UZITO GROUP B

      Sweetcorn; inazuia uzalishwaji wa insulin, inaingilia ufanisi wa kimetaboliki.

      Lenti; inasababisha sukari kushuka, inazuia virutubisho kufika mwilini vizuri, inaingilia ufanisi wa kimetaboliki

      Karanga; inaingilia ufanisi wa kimetaboliki, inashusha sukari, inazuia ufanisi wa kazi wa ini

      Mbegu za ufuta; zinaingilia ufanisi wa kimetaboliki, zinasababisha kushuka kwa sukari.

      Ngano; inazuia ufanisi wa kimetaboliki, inashusha sukari, inasababisha chakula kutunzwa kama mafuta badala ya energy (nguvu)

VYAKULA VINAVYOWAPUNGUZIA UZITO GROUP B

Mboga za majani, nyama, maini, mayai; yanasaida ufanisi wa kimetaboliki

ULAJI WA CHAKULA KWA GROUP B

      VYAKULA VYA NYAMA VYENYE UMUHIMU; kondoo, sungura

      VYAKULA VYA NYAMA VYA KUEPUKA; nguruwe, kuku, moyo, bata, quail, patridge.

      VYAKULA VYA BAHARINI; ni vizuri kwa type B

      VYAKULA VYA BAHARINI VYA KUEPUKA; barracuda, kaa, crayfish, lobster, pweza, Kamba (prawns), smoked salmon.

      VYAKULA VITOKANAVYO NA MAZIWA VYENYE UMUHIMU; jibini, maziwa ya mbuzi, skimmed milk, mtindi

      VYA KUEPUKA; ice-cream.

      OIL & FAT YENYE MANUFAA; mafuta ya zeituni.

      MAFUTA YA KUEPUKA; corn oil, mafuta ya mbegu za pamba, mafuta ya njugu, mafuta ya alizeti, ufuta.

      MBEGU; mara nyingi sio nzuri kwa B, ila waepuke korosho, karanga na siagi yake, ufuta, alizeti

      MAHARAGWE YENYE MANUFAA; maharagwe ya figo, maharagwe ya lima, navy beans.

      MAHARAGWE YA KUEPUKA; adzuki beans, maharagwe meusi.

      NAFAKA ZENYE MANUFAA; mtama, oat bran, mchele.

      NAFAKA ZA KUEPUKA; ngano, cornflakes, corn meal.

      MBOGAMBOGA ZENYE MANUFAA; Brussel, kabichi, karoti, koulifulawa, kale, uyoga, haradali, parsley, pilipili, viazi vitamu, magimbi.

      MBOGAMBOGA ZA KUEPUKA; parachichi, zeituni, boga, sweetcorn, tofu, nyanya.

      MATUNDA YENYE MANUFAA; ndizi mbivu, cranberries, zabibu, papai, nanasi.

      MATUNDA YA KUEPUKA; nazi, komamanga, starfruit, prickley pears.

      VIUNGO; waepuke kutumia mdalasini.

      VINYWAJI VYENYE MANUFAA; green tea

      VINYWAJI VYA KUEPUKA; spirits, soda

BLOOD GROUP AB (The Enigma)

       Mchanganyiko wa A na B

       Tabia kama za kinyonga, kwenye kukabiliana na mazingira au milo yao

       Wana mfumo wa kula ambao ni sensitive.

       Kinga yao ipo kimya sana.

       Wanadili na stress kwa kiroho Zaidi, mazoezi na ubunifu

       Wana risk kubwa ya saratani kwa sababu wana mchanganyiko wa A na B, hivyo mbaya wa B na mbaya wa A, kwa AB anaweza kua rafiki.

       Kinga yao haijatulia (compex), hii ni sifa inayowapa wengine Nguvu na wengine udhaifu.

VYAKULA VINAVYOWAONGEZEA UZITO GROUP AB

       Nyama nyekundu; mmeng‘enyo wake ni wa tabu na inahifadhiwa kama mafuta.

       Kidney beans, lima beans, mbegu, sweetcorn (nafaka au mahindi yaliovunwa kabla ya kukomaa), ngano; zinazuia kuzalishwa kwa insulin hivyo kushuka kwa sukari

       Ngano; inashusha ufanisi wa kimetaboliki na utumiwaji wa kalori.

VYAKULA VYA KUPUNGUZA UZITO KWA GROUP AB

       Tofu, vyakula vya baharini, mboga za majani; zinasaidia ufanisi wa kimetaboliki.

       Kelp, vyakula vya maziwa; vinaongeza ufanisi wa kuzalishwa kwa insulin.

       Matunda ya alkaline (zabibu, nanasi, tikiti maji,apple n.k); yanaongeza alkaline kwenye misuli.

       Nanasi; linasaidia mmeng‘enyo wa chakula, inaongeza ufanisi wa ufanyaji kazi wa tumbo.

ULAJI WA VYAKULA WA GROUP AB

       NYAMA ZENYE MANUFAA; kondoo, sungura, turkey (Bata Mzinga).

       NYAMA ZA KUEPUKA; nyama ya ng‘ombe, nyama ya nyati, kuku, bata, nguruwe, moyo, quail.

       VYAKULA VYA BAHARINI VYENYE MANUFAA; tuna, cod, mackerel, red fish, grouper, mahi mahi.

       VYAKULA VYA BAHARINI VYA KUEPUKA; barracuda, kaa, crayfish, lobster, pweza, chaza (oysters), smoked salmon (samaki saroni).

       VYAKULA VYA MAZIWA; mayai ni mazuri kwa AB, jibini ya cottage, jibini ya farmers,

       VYAKULA VYA MAZIWA VYA KUEPUKA, jibini ya bluu, brie, siagi, maziwa ya siagi, ice-cream,

       MAFUTA YENYE MANUFAA; mafuta ya zeituni

       MAFUTA YA KUEPUKA; corn oil (mafuta ya nafaka), mafuta ya mbegu za pamba, mafuta ya alizeti, mafuta ya ufuta.

       MBEGU ZENYE MANUFAA; chestnuts, karanga na siagi yake, walnuts

       MBEGU ZA KUEPUKA; hazelnuts, mbegu za poppy, mbegu za maboga, mbegu za ufuta, mbegu za alizeti.

       MAHARAGWE YENYE MANUFAA; lenti, navy beans, maharagwe ya pinto, maharagwe mekundu, maharagwe ya soya.

       MAHARAGWE YASIYOFAA; adzuki, maharagwe meusi, maharagwe ya figo, maharagwe ya lima.

       NAFAKA ZINZOFAA; mtama, oat bran, rice bran, mchele, *kwa wenye pumu (asthma) wanatakiwa wasitumie ngano kwa sababu inachochea kuzalishwa kwa mucus kwenye mfumo wa hewa, unga wa oat, unga wa mchele

       NAFAKA ZA KUEPUKA; ngano, cornflakes, cornmeal

       MBOGAMBOGA ZENYE MANUFAA; alfalfa, broccoli, koulifulawa, tango, kitunguu swaumu, kale, uyoga, haradali, parley, tofu, magimbi.

       MBOGAMBOGA ZA KUEPUKA; parachichi, pilipili ya chili, zeituni, sweetcorn.

       MATUNDA YENYE MANUFAA; cherries, mtini (fig), zabibu,

       MATUNDA YA KUEPUKA; ndizi, nazi, pera, maembe, komamanga, prickly pears, starfruit.

       VIUNGO VYENYE MANUFAA; curry powder, parley,

       VIUNGO VYA KUEPUKA; almond (mlozi) cornflour, corn syrup, pilipili.

       VINYWAJI VYENYE MANUFAA; kahawa, green tea

       VINYWAJI VYA KUEPUKA; spirit, chainyeusi,soda

Tukumbuke kua, vyakula vyenye manufaa ni vile ambavyo ni kama dawa, vyakula vya upande wowote (neutral) ni ambavyo ni vyakula tu, na vyakula vya kuepuka ni ambavyo ni kama sumu. Hivyo kama kuna vyakula sijavitaja, ujue hivyo ni neutral, na unaweza tu kutumia kama kawaida. Lakini vya kuepuka ujue kwako vina madhara Zaidi kuliko faida.

Pia najua unaweza usiifwate nadharia hii kwa 100%, lakini unaweza kujitahidi kwa kiasi flani, haswa haswa kama unasumbuliwa na magonjwa mbali mbali au kama unapata changamoto katika kupungua uzito.

FOOD IS MEDICINE, chakula sahihi ndio dawa ya kwanza kabla ya dawa nyingine yoyote ile, ndio maana watu ambao wanakula mlo sahihi, hua hawasumbuliwi na magonjwa, kua na uzito mkubwa na hua miili yao ina nguvu sana kulinganisha na weingine.

kwa msaada Zaidi juu ya nadharia (theory hii) unaweza kusoma kitabu kinachoitwa EAT RIGHT FOR YOUR BLOOD TYPE kilichoandikwa na Dr Peter D’Adamo 1996

Nadharia hii haijathibitishwa kabisa kitaalam, ingawa baadhi ya tafiti zinasema kua watu wengi imewasaidia

Hivyo unaweza kuitumia au usiitumie, cha msingi ni kuzingatia ulaji sahihi na kuepuka ulaji mbovu kwa ajili ya afya zetu.

Imeandikwa na SAMUEL MACHA

FIT BY WAYNE.

CONTACTS:

Mobile: 0753068572

Whatsapp: 0621068072 WHATSAPP

Comments

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed