Skip to main content

VYAKULA VINAVYOTUNZA AFYA YA NGOZI (ANTI-AGING FOODS)

 


VYAKULA VINAVYOHITAJIKA KATIKA AFYA YA NGOZI. (ANT-AGING FOODS)

Bila shaka unafaham ya kwamba kuna watu ambao wamekua na makunyanzi na kuonekana wakubwa (wazee) kuliko umri wao halisi.

Lakini pia kuna ambao ngozi zao hulegea baada ya kupungua na kuonekana kusinyaa pamoja na makunyanzi.

Collagen nip rotini muhimu sana katika kuipa ngoz afya, na ndiyo inayohusika na kufanya ngozi iwe na hali ya kuvutika (elasticity)

Lishe inahusika sana kwa kiasi kikubwa kufanya ngozi yako iwe vizuri na isiwe na makunyanzi au kuonekana yam zee kuliko umri wako.

VYAKULA MUHIMU KWA AFYA YA NGOZI.

·         KITUNGUU SWAUMU: kina kiwango kikubwa cha sulfur inayosaidia kuzalisha kiwango cha collagen. Hivyo jitahidi kutumia kitunguu swaumu kama moja ya viungo vyako muhimu.

·         MAHARAGE: protini itokanayo na maharage husaidia kuongeza kiwango cha collagen, bakuli moja la maharage lina wastani wa gram 15 za protini ambazo zikifanyiwa mmeng'enyo wa chakula, amino acids zinatumika kutengeneza collagen.

·         PILI-PILI HOHO: zina wingi wa Vitamin C ambayo husaidia kuzalishwa kwa collagen, husaidia ngozi ipone haraka inapopata jeraha. Vile vile hupambana inflammation hivyo kufanya ngozi isionekane kuzeeka haraka.

·         NYANYA: zina wingi wa Vitamin C pamoja na Lycopene ambayo hutumia kufanya refreshment ya ngozi na kufanya usionekane mzee au kua na ngozi yenye makunyanzi.

·         KUKU: nyama hii inawingi wa Niocene pamoja na Vitamin B6 pamoja na kiwango kikubwa cha protini. Hizi zote husaidia katika uzalishwaji wa collagen.

·         SAMAKI: sehemu kubwa ya samaki inayozalisha collagen ni kichwa, macho pamoja na mifupa yake. Lakini pia ngozi ya samaki ina kiwango kikubwa cha collagen. Ngozi yake ina kiwango kikubwa cha collagen peptides.

·         MAYAI: sehemu nyeupe ya yai ina kiwango kikubwa cha proline, ambayo ni amino acid inayosaidia uzalishwaji wa collagen.

Hivyo mtu anayeweza kutumia vyakula hivi atapata kiwango kikubwa cha collagen. Na ukiwa na kiwango kikubwa cha collagen, inakufanya uonekane mdogo Zaidi kwa sababu afya ya ngozi yako inakua nzuri sana.

EPUKA VYAKULA HIVI UKITAKA NGOZI NZURI

·         SUKARI: inaongoza kwa kufanya ngozi ionekane ya kizee au kuzeeka mapema kwa sababu inaingilia kazi ya collagen na elastin. Sukari inapovunjwa mwilini, hujishikiza na collagen na kusababisha makunyanzi. Lakini pia kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu hufanya mtu kuzeeka haraka na kuongezeka uzito.

·         ENERGY DRINKS: zimejaa sana kiwango kikubwa cha acids, sukari na kemikali nyingine ambazo ni mbaya. Zina kiwango kikubwa cha sodium na caffeine zinazosababisha ngozi kukosa maji (dehydration).

·         VYAKULA VINAVYOKAANGWA NA MAFUTA MENGI: hivi hua na kitu kinaitwa ADVANCED GKYCATION END PRODUCTS ambazo zinakufanya uzeeke haraka.

·         FAST FOODS (chipsi, pizza, burger): zina kiwango kikubwa cha Transfats zinazosababisha mishipa ya dam kuziba na kusababisha mlundikano wa mafuta kwenye mishipa ya damu.

·         POMBE: hushusha ufanisi wa ini ambalo ndio kiungo kikubwa cha kuufanyia mwili wako Detox. (kuondoa taka mwili). Hii husababisha kupata makunyanzi mapema.

·         VYAKULA VYENYE PILI PILI NYINGI: husababisha hali iitwayo ROSACEA kwenye ngozi.

·         WANGA AU NGANO ILIYOKOBOLEWA: unapokula hizi, zisipotumika mwilini hugeuzwa na kua sukari na husababisha kua na kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu. Na hii hupelekea kua na makunyanzi.

·         VYAKULA VYENYE CHUMVI NYINGI: husababisha kua na kiwango kikubwa cha sodium na kusababisha kitu kinachoitwa WATER RETENTION (maji kubaki mwilini). Na kusababisha ngozi iwe ya kizee kuliko umri wako. Ndio maana detox diet nyingi hua hazina chumvi, au chumvi kidogo sana.

Lakini juu ya haya yote, jitahidi sana kunywa maji mengi. Yanafaida kubwa sana kwenye afya ya ngozi na mwili kwa ujumla.

Ngozi nzuri pia ina ambatana na mazoezi. Sio lazima ufanye mazoezi makali, unaweza hata ukawa unatembea nusu saa kwa siku. Hii itasaidia sana misuli iweze kua active na kuchangamsha mwonekano wa ngozi yako.

Endelea kula vizuri, kumbuka ROMA HAIKUJENGWA KWA SIKU MOJA. Hivyo usichoke kula vizuri. Kwani ndio unajenga mwili wako uwe na afya bora.

Imeandikwa na SAMUEL MACHA.

FIT BY WAYNE.

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77

Hormonal Imbalance, Visababishi na Tiba yake

  Hormonal Imbalance HORMONAL IMBALANCE    Hormonal imbalance ama kwa Kiswahili ni mvurugiko wa kichochezi (hormone). Mara nyingi huwakumba wanawake Zaidi, ingawa hata wanaume wanaweza kua na tatizo hili. na kusababisha kiwango kidogo sana au kikubwa sana cha hormone au kichochezi chochote kutokukaa sawa.  NINI HUSABABISHA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Ulaji Mbovu wa chakula 2️⃣Unene (uzito uliopitiliza) 3️⃣Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.  4️⃣Stress na msongo wa mawazo 5️⃣kisukari 6️⃣Hyperglycemia (uzalishwaji wa kuzidi wa glucagon) 7️⃣Hypoglycemia (insulin kuzalishwa nyingi kuliko glucose kwenye damu) 8️⃣Saratani pamoja na vimbe kwenye via vya kizazi.  DALILI ZA HORMONAL IMBALANCE  1️⃣Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa 2️⃣Kutokushika mimba (infertility) 3️⃣Kutokua na uwezo wa kusimamisha uume 4️⃣Mbegu za uzazi kuwa chache (low sperm count) 5️⃣Uke kua mkavu (vaginal dryness) 6️⃣Kubadilika badilika kwa mzunguko wa hedhi au maumivu makali 7️⃣Kutokupata usingizi vizuri 8️⃣Kuongezeka uzito

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Kukaa sehemu moja kwa muda mrefu au kutokufanya mazoezi. (sed