Skip to main content

MSIMU WA SIKUKUU NITUMIE DIET GANI?

 

NITUMIE DIET GANI MSIMU WA SIKUKUU?❔❓❔❓

kama umekua ukitumia diet ya aina flani kwa ajili ya kupungua uzito (na kueka afya nzuri kwa ujumla), basi utakua umeshajiuliza swali la namna hii. 

Huu ndio ule msimu ambao kila kona unayopita wamepika chakula ambacho wewe ukitumia ni kinyume na Diet ambayo unaitumia katika kupungua uzito.

ONDOA SHAKA... FANYA YAFUATAYO:

Kabla ya yote, ni vyema ukafahamu ya kwamba ROME WAS NOT BUILT IN ONE DAY. Yaani Mji wa Roma haukujengwa ndani ya siku moja. bali ni mkusanyiko wa siku nyingi za ujenzi ndipo mji ukakamilika.

hivyo, hata kwa mtu ambae ana uzito mkubwa leo hii. sio kwamba aliongezeka ndani ya siku moja. Bali ni mkusanyiko wa siku nyingi ambazo hakua anakula vizuri au kua na mtindo mzuri wa maisha.

POINT YANGU NI IPI HASWA❓❔

kula kawaida siku ya siku kuu au msimu wa siku kuu hakutakufanya uharibu Diet yako ambayo umekua ukiendelea nayo. Hivyo bado unaweza kujumuika na ndugu jamaa na marafiki na mkala, kunywa na kufurahi pamoja.

ZINGATIA MAMBO YAFUATAYO🔰

1. Kula na ufurahie kinlichopikwa au utakachopika na kuandaa na wale uwapendao.

2. Baada ya msimu wa sikukuu kuisha, basi kesho yake rudi kwenye diet yako ya kuendelea na safari ya kua FIT pamoja na mwonekano mzuri.

3. Usisahau ya kwamba lengo lako ni lipi. hivyo ni vyema kurudi kwenye diet yako ya kupungua na kua na afya njema.

4. YOU ARE WHAT YOU EAT, vile unavyokula kila siku ndivyo hivyomutakavyokua.

5. Kumbuka ya kwamba, sio lazima uache Diet yako kwa msimu wa sikukuu, kama unaweza kuendelea hata kama ni sikukuu. Basi wewe ni Champion wa nguvu kwenye safari hii. kwani une nidhamu ya hali ya juu, na ni rahisi kushinda vita dhidi ya uzito mkubwa.

Kufikia hapo nikutakie maandalizi mema ya siku kuu ambazo zinakuja. nakutakia kheri, baraka pamoja na afya njema. (endapo utaitunza afya yako😉)

kwa msaada zaidi juu ya kupunguza uzito uliozidi, 

whatsapp 0621068072 (wa.me/255621068072), mobile 0676068572/0753068572

By SAMUEL MACHA

FIT BY WAYNE




Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

DETOX YA SIKU 7. HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE

  HATUA YA KWANZA KUPUNGUZA UNENE. Uzito Unaotakiwa kua nao Kulingana na Urefu Pamoja na Jinsia UREFU (CM) UREFU (FT & INCH) UZITO (KG)       MWANAUME MWANAMKE 147 4' 10" - 45-59 150 4' 11" - 45-60 152 5' 0" - 46-62 155 5' 1" 55-66 47-63 157 5' 2" 56-67 49-65 160 5' 3" 57-68 50-67 162 5' 4" 58-70 51-69 165 5' 5" 59-72 53-70 167 5' 6" 60-74 54-72 170 5' 7" 61-75 55-74 172 5' 8" 62-77 ...

BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI

 BAWASIRI NA JINSI YA KUITIBU KWA NJIA ZA ASILI.   💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊💊   BAWASIRI NI NINI?   Bawasiri (kikundu, future, puru au mjiko ) ni hali ya kutuna kwa mishipa ya damu katika mfereji wa sehemu ya haja kubwa (anus). Kuna aina mbili za Bawasiri;   1. Bawasiri za ndani ( internal haemorroids )   2. Bawasiri za nje ( external haemorroids )  Bawasiri za ndani hua na dalili ya kupata kinyesi kilichokua na damu,  bawasiri za nje hua na dalili ya maumivu makali wakati wa kujisaidia pamoja na kinyama kutoka kwa nje.  NINI VISABABISHI VYA BAWASIRI?   1️⃣Historia ya familia, mara nyingi baadhi ya familia hukumbwa na changamoto hii. Na hua watu wa familia hiyo husika wanakua na hili tatizo. 2️⃣Kupata choo kigumu mara kwa mara husababisha mtu kutumia nguvu nyingi (straining) ambayo husababisha bawasiri kutokea. 3️⃣Unene (uzito uliopitiliza) hua ni kisababishi cha bawasiri kwa sababu ya kuongezeka kwa Rectal Vein Pressure. 4️⃣Ku...

CALORIE ZA VYAKULA VYA TANZANIA

 CALORIES ZA VYAKULA TANZANIA   NINI MAANA YA CALORIE?    Calorie ni kiasi cha nishati kinachohitajika ili kuongeza joto la gramu moja ya maji (°C). Kwa lugha nyepesi, calorie katika chakula hutoa nishati (energy) kwa njia ya joto ili miili yetu iweze kufanya kazi. Hii ni kwa sababu miili yetu huhifadhi na kuchoma calorie kama mafuta.  UHUSIANO WA CALORIE NA UZITO WA MWILI.  Kwa kawaida, kila chakula kina kiwango chake cha calorie. Hivyo unapokula chakula, unaingiza mwilini calorie kadhaa, na mwili wako pia unatumia calorie katika kuweka uhai. Lakini unapokula chakula, unaingiza calorie mwilini. Na mwili wako pia unatumia calorie kama nishati. Hivyo unapokula calorie nyingi kuliko mwili unavyoweza kutumia, zinahifadhiwa kama mafuta na utaongezeka uzito. Unapotumia calorie nyingi kuliko unavyoingiza mwilini, unapungua uzito. Na ukitumia kiasi sawa na unachoingiza, basi unabaki na uzito ule ule.   MWANADAMU ANAHITAJI WASTANI WA CALORIE NGAPI? ...