Skip to main content

Posts

Showing posts from June, 2022

USITUMIE DAWA ZA MAUMIVU AU ANTIBIOTIKI PASIPO SABABU ZA MSINGI

  USITUMIE DAWA ZA MAUMIVU PASIPO SABABU ZA MSINGI. Mara nyingi dawa hua hazitibu au kuondoa tatizo, bali zinatuliza dalili ambazo zinatokana na tatizo husika. Dawa za antibiotic hua zina ufanisi kwa sababu hua zinaenda kuangamiza vimelea vinavyosababisha ugonjwa, ila shida yake ni moja, hua zinaangamiza pia bacteria wazuri ambao wapo ndani ya mwili wako. Ndio maana ni busara sana kama umetoka kutumia dawa za antibiotic kwa ajili ya matibabu, uwe unatumia vyakula vichachu (fermented foods), mfano maziwa ya mtindi ili kuweza kurudisha uwiano wa bacteria wazuri katika tumbo. Usitumie antibiotic, dawa za maumivu au antacids kwa Zaidi ya siku 5 mfululizo. Kwani utaangamiza bacteria wako wazuri katika tumbo, ambao ndio wanaosaidia kuweka mwili wako sawa. Ni vyema kujua haswa chanzo cha tatizo ni nini, badala ya kukimbilia kumeza dawa. Usiwe mtumwa wa madawa. Kila dawa unayomeza inakuachia sumu mwilini mwako. Kumbuka ya kwamba CHEMBE NA CHEMBE MKATE HUWA . Na SAMUEL MACHA FIT B

BAWASIRI NA JINSI YA KUJITIBU UKIWA NYUMBANI.

  BAWASIRI NA JINSI YA KUKABILIANA NAYO NYUMBANI. Bawasiri ni sehemu katika njia ya haja kubwa mwishoni (rectum) au dalili ya tatizo lenyewe. Mishipa ya fahamu ya Bawasiri (Haemorrhoidal Plexus): ni mfumo wa mishipa ya fahamu, mishipa ya damu, tishu pamoja na misuli laini. Haemorroidal Plexus ni kama sehemu laini ambayo husaidia kudhibiti haja kubwa wakati wa haja kutokana na mgandamizo mkubwa unaokuepo katika tumbo. Plexus hii pia huhakikisha ya kwamba njia ya haja kubwa (anus) hufunga vizuri wakati mtu amepumzika au ametulia Kuna aina mbili za haemorroidal plexus.         I.             Internal plexus       II.             External plexus External plexus (mishipa upande wa nje) zina mishipa wakati internal plexus haina mishipa ya fahamu. Hivyo external plexus (mishipa ya nje) hua na maumivu makali wakati ya ndani haina maumivu. Mishipa hii (haemorroids) huleta dalili pale zinapotanuka, kuvimba au kutokezea kwa nje ya njia ya haja kubwa. Mtu anapokua katika sababu

UKWELI KUHUSU NJIA ZA UZAZI WA MPANGO

  Njia za uzazi wa mpango Ukweli Kuhusiana Na Njia za Uzazi wa Mpango. Kuna aina 2 kuu za njia za uzazi wa mpango. 1.       Combined Oral Contraceptives (progesterone and oestrogen) 2.        Progesterone only contraceptives (POC) Hua zinakuja katika hali tatu tofauti. 1.       Vidonge vya kumeza. (ikijumuisha na P2) 2.       Sindano ambazo mtu huchomwa kila baada ya miezi 3 3.        Long acting mfano Norplant or jadelle (vitanzi) Njia hizi huzuia mbegu zisirutubishe yai katika mirija ya uzazi wakati wa ovulation. Hivyo hufanya kazi ya kuzuia ovulation kwa mwanamke. Mwanamke anapomeza dawa hizi, hutuma taarifa hasi (negative feedback) kwenye hypothalamus (sehemu ya ubongo) ambapo hupunguza uzalishwaji wa follicle stimulating hormone (FSH) pamoja na Lutenizing Hormone (LH), ambapo hufanya au kuzuia ukuaji wa follicle. Follicle ni kimfuko ambacho hua na yai ambalo halijakomaa. Isipotumika, basi yai hilo hupoteza uhai na mwanamke atakosa ovulation yake na kutokua na fer