Skip to main content

Posts

Showing posts from March, 2021

VIRUTUBISHO 6 VYENYE AFYA

  VIRUTUBISHO 6 VYENYE AFYA Virutubisho ni dutu (substance) ambazo hurutubisha mwili na afya kwa ujumla. Virutubisho hupatikana kwenye vyakula tunavyokula au kunywa kila siku.  Japokua, kila tunachokula au kunywa, hytofautiana virutubisho vinavyopatikana. Kuna ambavyo vimejaa virutubisho, na kuna ambavyo havina virutubisho na hivyo kua havina faida kwenye mwili wa mwanadamu ingawa vinaonekana kua na ladha nzuri. VIRUTUBISHO 6 VYENYE AFYA NA VYAKULA VYAKE. 1. NYUZI NYUZI Nyuzi nyuzi husaidia sana kuratibu uzito wa mwili, kupunguza hatari za kisukari na lehemu (cholesterol) kwenye damu, Pia kupunguza athari za magonjwa ya moyo. Nyuzi zisizo yeyuka husaidia sana kuweka mfumo wa chakula na msukumo uende kwa urahisi. vyakula Vyenye nyuzi nyuzi ni kama vile Njegere, karoti, maharage mabichi, cauliflower, viazi vitamu, matunda 2. VITAMIN A Husaidia sana kuona kwa macho na kukinga mwili dhidi ya magonjwa ya kuambukiza. Pia husaidia kuwezesha nyama za mifupa, ngozi na meno kuwa na afya nzuri.

ASALI NA LIMAO KATIKA KUPUNGUZA UZITO

  Asali na Limao ASALI NA LIMAO KATIKA KUPUNGUZA UZITO. Kuna mengi sana yanasemwa kuhusiana na asali. Wengine husema asali huongeza uzito kama sukari, na wengine husema ya kwamba asali hupunguza uzito. lakini je, ukweli haswa ni upi? Kwa kawaida, ni kweli ya kwamba asali ina calories nyingi. Asali ina calorie 304 katika kila gram 100. Hivyo ni kiasi kikubwa. lakini vile vile, Asali ikitumika katika mchanganyiko wake maalum, inaweza kukusaidia kupunguza unene, uzito pamoja na kitambi au nyama zembe endapo utatumia mara kwa mara. (IFAHAMIKE YA KWAMBA, HUWEZI KUPUNGUA UZITO KAMA HUBADILISHI MTINDO WAKO WA KULA NA MAISHA) Hapa tutatumia mchanganyiko maalum kwa ajili ya kukusaidia kuweza kupunguza uzito, kitambi pamoja na unene kwa ujumla. Japokua mchanganyiko huu una faida nyingine nyingi, ila kwa sasa nitaelezea kuhusiana na uzito. MAHITAJI YA MCHANGANYIKO WAKO Asali mbichi kijiko kimoja cha chai Maji ya vuguvugu kikombe 1 Vijiko 2 vya maji ya limao JINSI YA KUTENGENEZA Chukua limao lako

SABABU 15 KWA NINI UNAONGEZEKA UZITO.

  kwa nini unaongezeka uzito. SABABU 15 KWA NINI UNAONGEZEKA UZITO yawezekana umekua ukifanya mazoezi na kutafuta njia kadhaa za kuweza kupunguza uzito ambao umezidi, ila mara nyingi unakwama na hufikii malengo yako. Huenda ni kwa sababu hujazijua sababu hizi zinazosababisha kuongezeka kwa uzito. 1. KUTOKUPATA USINGIZI WA KUTOSHA Haswa wakati wa usiku, hii husababisha kitu kinaitwa LOWER RESTING METABOLIC RATE 2. MVURUGIKO WA HOMONI (HORMONAL IMBALANCE) Homoni au vivhochezi ndio husaidia kukontrol mwili na yanayotokea mwilini, hivyo zinapokua hazipo katika uwiano unaotakiwa, hupelekea mwili kuongezeka uzito kwa baadhi ya watu. 3. WATER RETENTION (MAJI YANAYOBAKI MWILINI BILA KUTOKA) Mwili wako unapohifadhi maji mwilini bila kutumika, utagundua ya kwamba uzito unaongezeka. Hii ni kwa sababu maji pia yana uzito, hivyo yanavyozidi kua mengi mwilini, na uzito unaongezeka. Moja ya sababu zinazopelekea hali hii ni utumiaji wa chumvi nyingi, pia baadhi ya dawa, kubadilika kwa homoni, au baadh