Skip to main content

Posts

Showing posts from June, 2023

JINSI YA KUZUIA NA KUKABILIANA NA TATIZO LA VIMBE KWENYE KIZAZI (FIBROIDS)

  JINSI MWANAMKE ANAVYOWEZA KUZUIA AU KUKABILIANA NA VIMBE KWENYE KIZAZI (FIBROIDS). Fibroids ama vimbe kwenye kizazi ni tatizo la kihomoni ambalo linatokea kwa mwanamke ambae yupo katika umri wake anaoweza kuzaa. Hii humaanisha ya kwamba fibroids hua zinalishwa na homoni ya oestrogen. Fibroids ni kama magugu ambayo huota shambani katika shamba ambalo halifanyiwi palizi au limeachwa. Wanawake walio katika hatari ya kupata fibroids ni;- ·        Wanawake wenye umri kuanzia miaka 28, japokua hata chini ya miaka 28 wanaweza kupata. ·        Wanawake wanene. ·        Wanawake weusi (waafrika); hii ni kwa sababu ya ulaji pamoja na mtindo wa maisha. ·        Wanawake wenye shida ya presha pamoja na kisukari. ·        Historia ya familia kua na fibroids. Familia huambukizana epigenetics na endocrine disruptors kutokana na tabia ya ulaji na mtindo wa maisha ya familia husika. ·        Wanawake ambao hawajazaa. Haswa ambao wamefika miaka 30. ·        Wanawake wenye upungudu

JINSI YA KUZUIA NA KUKABILIANA NA UGONJWA WA GOUT.

  KUHUSIANA NA UGONJWA WA GOUT. Kuna component moja hujulikana kama FRUCTOSE . Hii ni component hatari sana katika afya ya mwanadamu, lakini cha kushangaza ni kwamba wanadamu wengi wanaitumia kwa kuifurahia bila kujua ya kwamba hii ni sumu ambayo inawamaliza taratibu. Fructose hupatikana katika sukari, asali pamoja na matunda matamu. Fructose inapoingia katika mwili, mchakato wake hufanyika katika ini tu. Na hutambuliwa na enzyme ijulikanayo kwa jina la FRUCTOKINASE . Kazi ya Fructokinase ni kufanya metabolism ya Fructose ili iweze kua FRUCTOSE 1 PHOSPHATE . Mchakato huu hupelekea enzyme nyingine kuamshwa ijulikanayo kama ADENOSINE MONOPHOSPHATE DEAMINASE ambayo hupelekea kuzalishwa kwa taka mwili ijulikanayo kama URIC ACID. URIC ACID ndio chanzo kikuu cha GOUT. Wengi watakwambia ya kwamba Gout inasababishwa na ulaji wa nyama nyekundu. Mtu akikwambia hivi, mwambie ya kwamba Gout inasababishwa na kuwepo kwa kiwango cha Uric Acid katika damu ambacho husababishwa na FRUCTOSE.