Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2022

JE, MAJI YA MOTO HUSAIDIA KUPUNGUZA KITAMBI?

  JE, MAJI YA MOTO HUSAIDIA KUPUNGUZA KITAMBI? Bila shaka umeshawahi kuona watu ambao hunywa maji ya moto na limao kila asubuhi huku wakisema ya kwamba wanafanya hivyo ili kupunguza kitambi. Cha ajabu ni kwamba watu hawa wanafanya hivi lakini hawafanyi mabadiliko yoyote juu ya vyakula wanavyokula au mtindo wa maisha. Kwa kifupi ni kwamba, ukiona mtu anasema anakunywa maji ya moto kwa lengo la kupunguza kitambi, ujue ni mvivu wa kubadilisha mtindo wake wa maisha na anapenda njia za mkato. Ila ukweli ni kwamba, katika kupunguza unene na kuondokana na kitambi, hua hamna njia za mkato. UKWELI KUHUSU MAJI YA MOTO Maji ya moto hayayeyushi mafuta kama wengi wanavyodhani. Na pia hayana mchango wowote katika kuyeyusha mafuta yanayosababisha unene mwilini mwa mwanadamu. Tindikali ya Hydrocloric tumboni ndio husaidia katika kumeng`enya chakula, lakini sio maji ya moto. Mtu anayekunywa maji ya moto na anayekunywa maji ya baridi, wote wanakunywa maji. Na hamna kitu cha ziada kinachowa

MADHARA YA UNENE KWA WANAWAKE

  MADHARA YA UNENE KWA WANAWAKE. Wanawake hupata madhara makubwa Zaidi kwa sababu ya unene ukilinganisha na wanaume. Ingawa ifahamike ya kwamba, unene una madhara na athari kubwa wa mtu yoyote bila kujali ni wa jinsia gani. NI KWA NINI MWANAMKE ANA ATHIRIKA ZAIDI? ·          MATATIZO YA UZAZI : wanawake wanene huwa wanakumbwa na changamoto nyingi za uzazi kutokana na kuvurugika kwa homoni pamoja na mzunguko wa hedhi. ·          KUPUNGUA KWA HAMU YA TENDO LA NDOA : mara nyingi huwalaumu wanaume kwamba wana uume mdogo au wanamwaga mapema. Lakini uhalisia ni kwamba wanawake wanene hua hawana hamu ya tendo la ndoa, ni ngumu kuamsha hisia zao za mahaba ukilinganisha na wanawake wenye uzito sahihi. ·          MATATIZO KATIKA KUJIFUNGUA: hua wanapoteza nguvu katika kusukuma mtoto wakati wa kujifungua. Au pia hua na watoto wakubwa (macrosomia) kutokana na athari za insulin kwa mtoto anaekua tumboni. ·          VISIRANI NA HASIRA ZISIZOKUA NA SABABU: wanawake wanene hua na self-es